OYA SISTA UKIGEUZA UZURI WAKO MTAJI, UTAISHIA KUCHEZEWA! - LEKULE

Breaking

18 May 2015

OYA SISTA UKIGEUZA UZURI WAKO MTAJI, UTAISHIA KUCHEZEWA!



Niaje…niaje wanangu na maduu wa ukwehe? Inakuwa nini watu wangu wa nguvu? Imekuwa fasta kinoma na tumekutana tena, huwezi kuamini kama kitu cha wiki kimekatika. Enewei ndo kama hivo kachala wako nipo chuma kabisa nimeshatokelezea rede kukisanua hapa kwa fasi ya jamvini. Wanangu kitu cha mvua kimezingua bati kwani kuna maproblemu? Hakuna tatizo. Basi jiti!

Tudei namaindi kukusanua na ishu moko hivi ambayo mazee naona kama inazidi kuwa majanga kwa deizi zijazo hapo fowadi kozi kuna maduu f’lani hivi amazing bati ndo tuseme tu inshoti kwamba wamejitoa kitu cha fahamu aisee.
Kuna mabebiz wakare ambao ukiwapiga chambo wewe mwenyewe masti usizi kozi ni kitu na boksi la ukweli kabisa.
Taipu ya mashori kama hao ni wale ambao wanajiona na wanajua wao ni sumu yaani kisu ileile.

Wenyewe wanabilivu kuwa kwa kujaliwa kitu cha uzuri na Saa Godi dheni wanatakiwa kuishi laifu klasiki yaani supa kitaani. Si unajua zile za kujiona wa kishua?Situwesheni kama hiyo mazee imewafanya baadhi ya makiksi wazuri wa tauni kuwakimbia masela wangu wa kitaani waliocheza nao ile michezo ya makidi kozi jamaa hawana mawe. Wanachokifanya ni kuwafungia vioo kama vile hawawaoni ndo ujue heshima pesa ndevu mwachie beberu!

Maduu wa dizaini kaa hiyo mkwanja ndo kila kitu so anapoibuka chalii na mkwanja mbuzi dheni wanamrespekti kinoma na kuonekana ndiye mwenye haki ya kufaidi vinono. Chezea kuwa na mawe weye? Narudia tena kuwa, kama msela huna hela, niamini mimi kuwa makiksi wote wakare tauni utaishia kuwaita mashemu wa ukwehe. Kaa humu wewe nikusanue acha kuishi kwa kupelekwapelekwe kimbulula. Shauri yako utapaki gari juu ya mawe ndani ya dakika sifuri dheni uanze kuzingua watu.

Kwa laifu staili hiyo ndo maana mashori wako tayari kwa kila mwenye mkwanja kumvulia mambo f’lani na kumuona kapuku hastahili kuwa na mbebiz mkare kama yeye. Oya wana hii ndo dunia ileile ya masela walewale na mshori walewale ambao wanasavaivu kwa kutazama tudei tu bila kujali kuna tumoro. Asikwambie kichwa hii ndo problemu kubwa ya wanangu wenyewe.

Unajua nawu nini kimehapeni kwa mashori wa dizaini hiyo? Wamechezewa hatare na ukimpiga chabo sasa ule ukare umetoka nduki. Anaposimama kwa kioo kujitazama anajuta anapojilinganisha na enzi zile za chuchu saa sita. Wale wanangu waliokuwa wakimingo na kuchili nao sasa hivi wameanza mbele. Bidada ukubwa huo na taimu inaenda, sanuka wewe!

Oya sista sikia, ukigeuza uzuri wako mtaji, utaishia kuchezewa kisha utaachwa taimu ikiwa imeenda na huwa fronti wala baki!Mmenisoma maduu wangu wa ukwehe? Kitu cha wikiendi hichoo…kama vipi neksi wiki. Nduki!

No comments: