Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Shamariwa ‘A’, Kata ya Igoma, Wilaya ya Nyamagana, jijini Mwanza, Julias Makoye (CCM), amekutwa amejinyonga juu ya mti ulio jirani na nyumba yake usiku wa jana.
Makoye aliyetangazwa mshindi wa kiti
hicho katika uchaguzi wa serikali za mitaa uliofanyika Desemba 14, mwaka
jana, ameuongoza mtaa huo kwa awamu ya pili baada ya kuongoza miaka
mitano iliyopita.
Mke wa marehemu, Ivona Polikalapo,
alisema saa 10 juzi jioni alimsikia mumewe akiongea na mtu kwenye simu
yake ya mkononi na kumsisitiza anahitaji mzigo wake wote.
“Jana
(juzi) saa 10 jioni nilimsikia mume wangu akiongea na mtu katika simu na
kutaka alipwe mzigo wake wote kutokana na kukaa muda mrefu, lakini
aliyekuwa akizungumza naye sikumfahamu ni nani,”:- Polikalapo.
Aidha, alisema ilipofika saa 10 alfajiri
ya jana, mbwa wao walisikika wakibweka kwa muda mrefu hali iliyomfanya
marehemu atoke nje kuangalia kilichopo katika banda lao la mifugo huku
(mke) akiendelea kuandaa chakula cha mifugo hao.
“Baada
ya mume wangu kuamka na kwenda kuangalia kilichopo nje, hakuweza
kurejea ndani hadi pale nilipotoka kwenda kumwaga uchafu shimoni
nikashangaa baada ya kumuona ananing’inia juu ya mti…nilipojaribu
kumuita hakuitika,” alisema.
Hata hivyo, mama huyo anasema haamini
kama mume wake amejinyonga bali kanyongwa kutokana na mti aliojitundika
kutoonekana kuwapo na jiwe la ‘sapoti’ ili kutekeleza azma yake hiyo
No comments:
Post a Comment