Hukumu dhidi ya Freema Mbowe ni Julai 17 - LEKULE

Breaking

19 May 2015

Hukumu dhidi ya Freema Mbowe ni Julai 17

HUKUMU ya kesi ya kumshambulia mwangalizi wa ndani wa uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 inayomkabili Mbunge wa Jimbo la Hai, Freeman Mbowe, iliyotarajiwa kutolewa jana katika mahakama ya Wilaya ya Hai, imeahirishwa  hadi Julai 17 mwaka huu baada Mbowe kushindwa kufika mahakamani.

Mbowe ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema),ilidaiwa  alishindwa kufika mahakamani n kutokana na kutoa udhuru wa kubanwa na kazi  za serikali likiwamo bunge la bajeti linaloendelea  Dodoma.

Hukumu ya kesi hiyo imeahirishwa kwa mara ya pili sasa.  Kwa  mara ya kwanza hukumu ilikuwa itolewe Mei 11 mwaka huu lakini ilishindikana baada ya Hakimu Mfawidhi, Denis Mpelembwa kuwa nje ya mahakama kwa shughuli za ofisi.

Akiahirisha  kesi hiyo, Hakimu Mkazi Mfawidhi  Mpelembwa alisema   alishindwa kufika mahakamani hapo kutokana na kubanwa na shughuli za serikali hivyo kupangiwa siku nyingine kwa ajili ya kusomewa hukumu.

Katika kesi hiyo ya jinai namba 73 ya mwaka 2011,  Mbowe akiwa mmoja kati ya wagombea ubunge wa   Hai, mwaka 2010,  anadaiwa kumshambulia Nassir Yamin katika Kijiji cha Nshara, Kata ya Machame Kaskazini, Wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro.


 Katika uchaguzi huo wa mwaka 2010, Mbowe alishinda kwa kupata kura 28,585 akifuatiwa na Fuya Kimbita (CCM) aliyepata kura 23,349,  Hawa Kihogo (UDP) kura 258 na Petro Kisimbo (TLP) 135.

No comments: