Waziri Wa Ujenzi, Uchukuzi Na Mawasiliano Profesa Mbarawa Amteua Bwana Masanja Kungu Kadogosa Kuwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu Wa TRL - LEKULE

Breaking

2 Feb 2016

Waziri Wa Ujenzi, Uchukuzi Na Mawasiliano Profesa Mbarawa Amteua Bwana Masanja Kungu Kadogosa Kuwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu Wa TRL



 WIZARA YA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI.

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa amemteua Bwana Masanja Kungu Kadogosa kuwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania (TRL), ambako anakwenda kuchukua nafasi ya Mhandisi Elias Mshana ambaye anastaafu hivi karibuni.

Kabla ya Uteuzi huo Bwana Masanja Kadogosa alikuwa Mkurugenzi Idara ya Mikopo Benki ya Rasilimali Tanzania (TIB). Uteuzi huo unaanza mara moja.

Imetolewa na;
Kitengo cha Mawasiliano Serikalini.
02 Februari, 2016.

No comments: