Polisi auwa na majambazi Tanga - LEKULE

Breaking

16 Feb 2016

Polisi auwa na majambazi Tanga



Askari wa jeshi la polisi Koplo George Braiton aliyepigwa risasi na majambazi wakati akikabiliana nao katika tukio la ujambazi lililotokea barabara ya sita na saba jijini Tanga amefariki dunia.

Koplo Braiton amefariki dunia wakati akipatiwa matibabu katika hospitali ya Mkoa wa Tanga,Bombo, akiwa na watu wengine wawili waliopigwa risasi katika tukio hilo.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga ACP.Mihayo Msikhela amesema kuwa bastola ilitumika kupoteza uhai wa Koplo George Braiton wa kituo cha polisi Chumbageni na kujeruhi raia wengine wawili ambao bado wanaendelea na matibabu katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Tanga.

Polisi wamesema walifanikiwa kuwakamata majambazi hao wakiwa na bastola waliyoitumia kwenye tukio hilo pamoja na visu wanavyovitumia kwenye matukio ya kihalifu.

Majirani waliokuwa wakiishi na Koplo Braitoni wamesema tukio hilo limewagusa,lakini wakaiomba jamii kuwafichua wahalifu kwa lengo la kukabiliana na vitendo hivyo.

Kolpo Braitoni anatarajiwa kusafirishwa kupelekwa mkoani Mara Februari 16 kwa ajili ya mazishi.

No comments: