Mikutano zaidi kutafuta suluhu ya mzozo wa Syria - LEKULE

Breaking

11 Feb 2016

Mikutano zaidi kutafuta suluhu ya mzozo wa Syria

mjumbe maalum wa UN kuhusu Syria Steffan Demistura katika mkutano wa Syria mjini Geneva hivi karibuni
Katika mkesha wa mkutano wa kimataifa hapo kesho Alhamisi jijini Munich kuhusu kuzindia mchakato wa amani nchini Syria, Uturuki imeendelea kufungia mpaka wake ma mia ya wakimbizi wanaokimbia mapingano ya majeshi ya serikali na waasi katika mji wa Aleppo.
Mji wa munichi nchini ujerumani unawapokea kesho wajumbe wa kimataifa wanaojumuika katika nchi 17 na mashirika ya kimataifa waliokubaliana mwezi Novemba mwaka 1015 jijini Vienna kuhusu dira ya kidiplomasia kuhusiana na mzozo wa Syria.
Mpango huo ulianzishwa kupitia azimio la baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa la Desemba 18, linaloomba pia uwepo wa mazingira ya mashirika ya misaada kufika katika maeneo ya miji iliozingirwa, pamoja na usitishwaji mapigano.
Kufuatia mkutano huo, serikali ya Washington imeiomba kwa mara nyingine tena Urusi inayosaidia kijeshi mashambulizi ya Utawala wa rais Assad kusitisha mara mara moja hususan katika jimbo la Aleppo.
Waziri wa mambo ya nje wa Marekani John Kerry ambae serikali yake inajitahidi kuwa karibu na serikali ya Moscou kwa ajili ya kupatikana kwa suluhu ya mgogoro wa Syria amesema wanaelekea Munich wakiwa na matumaini makubwa.
Mzozo wa Syria uliodumu sasa ni zaidi ya miaka 5, uliogharimu maisha ya watu takriban laki mbili na elfu sitini na kuwafanya wengine zaidi ya milioni moja kutoroka makwao.(VICTOR)

Kabla ya uzinduzi wa mkutano huo mratibu wa muungano wa upinzani nchini Syria Riyad Hijab atakutana jumatano hii jijini London na waziri wa mambo ya nje wa Uingereza Philip Hammond.
Wakati huo huo jijini Moscou itazinduliwa ofisi ya wawakilishi ya wakurdi wa Syria wanaoomba kuwakilishwa katika mazungumzo, jambo ambalo linatupiliwa mbali na serikali ya Ankara.
Na huko Hegue nchini Uholanzi waziri mkuu wa Uholanzi Mark Rutte atampokea waziri mkuu wa Uturuki Ahmet Davutoglu na kuzungumzia kuhusu suluhu ya mgogoro wa wakimbizi.
Swala hili litajadiliwa pia katika mkutano wa mawaziri wa nchi za kujihami wa nchi za magharibi Nato jijini brussels hii leo. Wajumbe katika mkutano huo watajadili pia kuhusu ombi la Ujerumani na Uturuki kuitaka Nato kuingilia kati mgogoro huo.
Waziri wa ulinzi wa Marekani Ashton Carter atajaribu kukazia muungano wa majeshi kuhusu kupambana na kundi linalojiita Islamic State linalotumia fursa ya mapigano kati ya serikali na waasi kukalia maeneo makubwa ya Syria.

No comments: