Askari wa Ufaransa wakipiga kambi karibu na hoteli ya Splendid, mjini Ouagadougou, Januari 16, 2016
Na RFI
Watu
wasiopungua 26, ikiwa ni pamoja na wageni wengi, wameuawa katika
shambulio la wanamgambo wa kiislamu lililoendeshwa Ijumaa hii dhidi ya
hoteli na mgahawa mjini Ouagadougou.
Upande wa
wauaji, wanajihadi wanne wameuawa. Operesheni ya kuwasaka wahalifu
ilioendeshwa na vikosi vya usalama Jumamosi hii katika mji mkuu wa
Burkina Faso haikufaulu kuwapata wauaji walio mafichoni.
Saa
chache kabla ya shambulio hilo la kigaidi kumalizika katikati mwa mji wa
Ouagadougou, idadi ya vifo bado haijawa sahihi. Wizara ya Mambo ya Nje
ya Ufaransa (Quai d'Orsay) imetangaza Jumamosi hii mchana kwamba raia
wawili wa Ufaransa wameuawa na mwengine mmoja amejeruhiwa. Kitengo cha
kupambana na ugaidi cha Ofisi ya mashitaka mjini Paris kimeanzisha
uchunguzi.
Operesheni
ilioendeshwa Jumamosi mchana imepelekea kuwaokoa watu 126, ikiwa ni
pamoja na wengine 150 waliojeruhiwa. Akitembelea katika hoteli ya
Splendid, Rais wa Burkina Faso Roch Marc Kaboré amesema watu wasiopungua
23 kutoka mataifa mbalimbali wameuawa. Kwa sasa, Waziri wa Mawasiliano
wa Burkina Faso, Rémi Dandjinou, amesema kuwa ripoti rasmi ya mwisho
inaeleza watu wasiopungua 26 wameuawa.
Kwenye
akaunti yake ya Twitter, Gilles Thibault, Balozi wa Ufaransa, amesema
kuwa shambulio hilo limesababisha vifo vya watu 2, na nchi wanakotoka
hazijafahamika, akibaini kwamba"watu 150 kutoka mataifa 18 waliokolewa
na kwa sasa wanapatishiwa huduma za mwanzo. "
Washambuliaji ni akina nani?
Upande wa
wauaji, wanajihadi wanne wameuawa katika hoteli ya Splendid na vikosi
vya usalama vya Burkina Faso, vikisaidiwa na vikosi vya Ufaransa na
Marekani. "Washambuliaji waliouawa ni pamoja na Mwarabu mmoja na
Waafrika wawili weusi", amesema Waziri wa Usalama, Simon Compaoré.
Kwa
mujibu wa afisa wa polisi nchini Burkina Faso, mwanamgambo wa nne wa
kiislamu ameuawa katika hoteli ya Yibi, ambapo alikua alikimbilia baada
ya operesheni ya vikosi vya usalama dhidi ya hoteli ya Splendid. Afisa
huyo amesema kuwa wanawake wawili walikuwa miongoni mwa wanamgambo hao.
Lakini
taarifa hii haijathibitishwa. "Hatuna taarifa yoyote ya wanawake hao,
lakini operesheni bado inaendelea", Alpha Barry, Waziri wa Mambo ya Nje
wa Burkina Faso ameiambia mchana RFI.
Kulingana
na taarifa za RFI, kundi hili la magaidi limekua likiundwa na watu
zaidi ya kumi na tano. Ikimaanisha kwamba wengi wao hawajapatikana.
Shambulio hili limedaiwa kutekelezwa na AQMi, kundi lenye mafungamano na Al-Qaeda, kwa niaba ya kundi la al-Mourabitoune.
No comments:
Post a Comment