Rais wa Iran apongeza kuondolewa kwa vikwazo - LEKULE

Breaking

17 Jan 2016

Rais wa Iran apongeza kuondolewa kwa vikwazo

Javad Zarrif
Rais wa Iran, Hassan Rouhani, amepongeza kutekelezwa kwa mkataba uliosaniwa kuhusiana na mpango wake wa Nuklia.
Rais Rouhani amesema kuondolewa kwa vikwazo ambavyo havikustahili dhidi ya serikali yake, kumeashiria mwanzo mpya wa maendeleo wa taifa lake.
Rais huyo amehutubia bunge la nchi hiyo baada ya shirika la umoja wa mataifa kuthibitisha kuwa Iran haikuwa inatengeneza silaha za nuklia, hali iliyopelekea vikwazo dhidi yake kuondolewa.
Mkutano kati ya Marekani
Rouhani amesema kile mtu amefurahia mkataba huo, isipokuwa wale aliowataja kama wachochezi wa kanda hiyo, Israel na wabunge kadhaa wenye msimamo mkali katika bunge la congress nchini Marekani.
Waziri wa mambo ya nje wa Marekani John Kerry amesema, tishio la Iran kutengeneza silaha za nuklia limpunguzwa lakini amesema wataendelea kuchunguza kwa umakini.

No comments: