Waziri Mkuu wa
Israel Benjamin Netanyahu, amesema Iran ingali na azma ya kuunda zana za
Nuklia na mjini Washington spika wa Paul Ryan wa chama cha Republican,
amesema Taifa la Iran ambalo linaongoza kwa ufadhili wa ugaidi, huenda
ikatumia fursa hiyo kuwafadhili vitendo vya kigaidi duniani.
Hatahivyo sio mataifa yote yaliochukizwa na mkataba huo .Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-Moon, ameitaja hatua ya kuondolewa kwa vikwazo dhidi ya Iran kuwa ya kihistoria, akisema kuwa pande zote zimetekeleza wajibu wao.
Mawaziri wa mambo ya nje wa Uingereza na Ujerumani nao wameitaja kuwa ushindi mkubwa wa juhudi za kidiplomasia.
No comments:
Post a Comment