Israel yachukizwa na kuondolewa kwa vikwazo - LEKULE

Breaking

17 Jan 2016

Israel yachukizwa na kuondolewa kwa vikwazo

Benjamin Netanyahu
Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu, amesema Iran ingali na azma ya kuunda zana za Nuklia na mjini Washington spika wa Paul Ryan wa chama cha Republican, amesema Taifa la Iran ambalo linaongoza kwa ufadhili wa ugaidi, huenda ikatumia fursa hiyo kuwafadhili vitendo vya kigaidi duniani.
Hatahivyo sio mataifa yote yaliochukizwa na mkataba huo .
John Kerry na Javad Zarrif
Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-Moon, ameitaja hatua ya kuondolewa kwa vikwazo dhidi ya Iran kuwa ya kihistoria, akisema kuwa pande zote zimetekeleza wajibu wao.
Mawaziri wa mambo ya nje wa Uingereza na Ujerumani nao wameitaja kuwa ushindi mkubwa wa juhudi za kidiplomasia.

No comments: