Hausigeli Afariki Kwa Kulawitiwa Na Bosi Wake - LEKULE

Breaking

27 Jan 2016

Hausigeli Afariki Kwa Kulawitiwa Na Bosi Wake


Mtumishi  wa nyumbani mwenye umri wa miaka 23, aliyekuwa akifanyakazi katika nyumba iliyo eneo la Mwika-Mrimbo, Moshi Vijijini, mkoani Kilimanjaro, amekufa kwa madai ya kulawitiwa na bosi wake, Zablon Shaaban (32).

Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani Kilimanjaro, William Nyello jana alithibitisha akisema tukio hilo ni la Januari 25, mwaka huu saa 3 usiku katika kata hiyo. 
Alisema mtumishi huyo wa nyumbani alifanyiwa kitendo hicho na bosi wake aliyekuwa akiishi naye baada ya kurejea nyumbani wakitokea matembezini jioni.

“Mtuhumiwa alikuwa akiishi na marehemu nyumba moja, waliporejea katika matembezi ya jioni na wakati wa kulala, mtuhumiwa alimfuata marehemu chumbani kwake na kumkaba koo na kumlawiti,” alisema Nyello.


Kaimu Kamanda alisema kutokana na kitendo hicho, kilichothibitishwa pia kwa uchunguzi wa daktari, polisi inamshikilia mtuhumiwa huyo na atafikishwa mahakamani.

No comments: