Huyu Ndiye Gabo Zigamba Mjukuu wa Mzee Kiyeyeu wa Iringa - LEKULE

Breaking

27 Jan 2016

Huyu Ndiye Gabo Zigamba Mjukuu wa Mzee Kiyeyeu wa Iringa

Gabo-zigamba-21
Gabo Zigamba mwigizaji wa filamu

UNAPOSIKIA jina la Gabo Zigamba si jina geni katika tasnia ya filamu , Gabo amejizolea umaarufu katika tasnia ya filamu baada ya kufanya vizuri na kuwachanganya wapenzi wa filamu Bongo, wengi wakiamini kuwa ni kijana wa Kimachinga kutoka Kusini kumbe ni Mdigo na Mhehe.

Jina halisi la msanii huyu ni Salim Ahmed Issa akisema hilo ni jina la kliniki, lakini jina la riziki anajulikana kama Gabo Zigamba, amezaliwa Mitaa ya Mshindo na kukulia katika mitaa ya Kitanzini kama ingekuwa hapa Dar ni mtoto aliyezaliwa Ilala na kukulia mitaa ya Kariakoo akilelewa na mama yake Rafia Issa Kiyeyeu.

Babu yake ni Mtogapaafwe Kiyeyeu familia ya Martin Kiyeyeu mtu maarufu sana Iringa ambaye kila unapotaja jina lake wengi ukumbuka kuhusu maajabu ya kaburi lake, Gabo anasema kuwa ameishii pande zote mbili lakini sehemu kubwa sana ni Iringa kwa mama yake akisoma Ipogolo Iringa.
Gabo anasema yeye ni mwanaharakati sauti ya wanyonge isiyosikika hivyo alianza harakati zake kitambo akifiria ni jinsi anavyoweza kufikisha ujumbe kwa jamii husika kwa kupitia sanaa na hasa filamu, wengi wanaamini kuwa sinema yake ya kwanza ni Bado Natafuta lakini ni kazi ilifanya vizuri baada ya kupewa nafasi.

SANAA ALIANZA LINI

Gabo kuigiza alianza kitambo lakini rasmi ilikuwa ni 2006 kwa kushiriki katika vikundi mbalimbali huku akiwa na shauku kubwa ya kuwa nyota na kufikia lengo lake la kuwatetea wasio na nafasi anasema haikuwa rahisi sana kwani kulikuwa na changamoto nyingi ambazo hazikumkatisha tamaa.
Harakati zangu hazikuja kama upepo sinema yangu ya kwanza ilikuwa ni Olopong iliyotengenezwa na Al Riyamy Production chini ya Khalfan Abdalah, hapo milango ndio ilifunguka kwani baada ya hapo nikacheza 007 Boyz,”anasema Gabo.


Baada hapo alishiriki katika filamu ya The Plan, na kujiunga na kampuni ya marehemu Juma Kilowoka ‘Sajuki’ Wajey Film akishiriki katika sinema zao kama mwigizaji na kufanikiwa kucheza filamu Mchanga na Keni, The killer na 007 Days alikuwepo hapo akijifunza vitu katika tasnia ya filamu.

No comments: