Wakazi zaidi ya 100 wa mtaa wa Kasera Kange jijini Tanga wameagizwa kuvunja nyumba zao kisha kuondoka - LEKULE

Breaking

31 Oct 2015

Wakazi zaidi ya 100 wa mtaa wa Kasera Kange jijini Tanga wameagizwa kuvunja nyumba zao kisha kuondoka

Wakazi zaidi ya 100 wa mtaa wa Kasera Kange jijini Tanga wameagizwa kuvunja nyumba zao kisha kuondoka mara moja katika eneo hilo kufuatia baadhi ya viongozi wa serikali kumega sehemu ya ardhi ya mwekezaji kisha kuwapatia wananchi.
Wakizungumza na katika eneo la tukio baadhi ya waathirika waliouziwa ardhi katika eneo hilo miaka saba iliyopita wamesema hawatakubali kuondoka katika mazingira ya utatanishi kwa sababu viongozi wa serikali ya mtaa wa kasera walipatiwa hati zinazowasaidia kuwatambulisha kuwa ni wamiliki halali wa eneo hilo.
 
Akijibu tuhuma za kuwauzia viwanja wakazi wake na taratibu zilizotumika kuwapatia hati miliki za serikali za mitaa,mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa Kasera Kange Bwana.Rajab Mbalazi amekiri kuwapatia ardhi wakazi hao isipokuwa baada ya wakazi kuanza kuchangamkia eneo hilo maafisa mipango miji waliwaagiza wananchi kuacha mara moja ujenzi wa nyumba ili kuepuka kubomolewa.
 
Kufuatia hatua hiyo mwekezaji wa eneo hilo Bwana.Danniel Mmbaga amesema kuwa eneo hilo wanalimiliki kisheria kwa mkataba wa miaka 99 hivyo amewaagiza wakazi hao hata kama wamejenga miundo mbinu katika eneo hilo ni vyema wakaondoka kabla sheria haijachukua mkondo wake.

No comments: