Taasisi ya mwalimu Nyerere yaitaka tume ya uchaguzi ZEC kuzingatia Sheria. - LEKULE

Breaking

31 Oct 2015

Taasisi ya mwalimu Nyerere yaitaka tume ya uchaguzi ZEC kuzingatia Sheria.

Taasisi ya mwalimu Nyerere imeitaka tume ya uchaguzi ya Zanzibar ZEC kufanya kazi kwa kuzingatia katiba ya nchi na sheria na sio kutanguliza mbele maslahi binafsi ya kisiasa hatua ambayo amesema inaweza kusababisha machafukona  umwagaji wa damu.
Akizungumza na vyombo vya habari mjini musoma,mmoja ya watu aliyewahi kuwa mshauri wa baba wa taifa hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ambaye pia ni mkurugenzi mtendaji wa taasisi ya Mwalimu Nyerere Bw.Joseph Butiku,amesema amekerwa na tabia ya ZEC kusitisha uchaguzi na kushindwa kuwatangazia wananchi kiongozi wao waliomchagua,huku ikishindwa kuheshimu matakwa ya wananchi walipiga kura  katika visiwa vya Zanzibar.
 
Aidha Bw.Butiku ambaye ni kada wa chama cha mapinduzi CCM amewataka wananchi wazanzibar kutokubali tena kurudia upigaji wa kura hadi hapo yatakapotolewa maelezo ya kuridhisha na wahusika waliosababisha  uchaguzi huo kufutwa pia waweze kuchukuliwa hatua kali za kisheria.
 
Kwa sababu hiyo amewataka viongozi kuheshimu sheria na katiba ya nchi na  kwamba chama ambacho kinadhani kimeshindwa katika uchaguzi huo kikubali   matokeo badala ya kuifanya zanzibar ni mali ya chama fulani pekeee.

No comments: