Tanzania kujenga bandari kubwa zaidi Afrika Mashariki - LEKULE

Breaking

17 Oct 2015

Tanzania kujenga bandari kubwa zaidi Afrika Mashariki


Bagamoyo
Mji wa Bagamoyo zamani ulitumiwa kuwazuilia watumwa kabla yao kupelekwa ZanzibarUjenzi wa bandari inayotazamiwa kuwa kubwa zaidi katika kanda ya afrika mashariki umeanza nchini tanzania.
Bandari hiyo inayojengwa katika mji wa bagamoyo itakuwa na uwezo wa kukimu mashehena milioni 20 kila mwaka, idadi ambayo ni mara mbili zaidi ya bandari inayotumika sasa jijini Dar es Saalam.
Mradi huo utagharimu takriban dola bilioni 11, huku ufadhili mkubwa wa kiasi hicho ukitoka nchini china.
Serikali ya Tanzania inasema kuwa mradi huo utaiwezesha kushindana na Kenya katika biashara za kikanda na rubaa za kimataifa.
Bandari hiyo inatarajiwa kutoa ushindani mkali kwa bandari iliyo mjini Mombasa katika taifa jirani la Kenya.
Mji wa Bagamoyo umo kilomita 75 kaskazini mwa Dar es Salaam na ndilo eneo anamotoka Rais Jakaya Kikwete anayeondoka mamlakani baada ya uchaguzi wa urais Oktoba 25.
Bagamoyo ulikuwa ndio mji mkuu wa awali wa kikoloni chini ya Wajerumani na ulikuwa kituo kikuu katika biashara ya utumwa. Watumwa waliwekwa katika mji huo kwa muda kabla ya kusafirishwa hadi soko kuu katika kisiwa cha Zanzibar.

No comments: