KUWA MSAIDIZI YANGA NI HATUA KWA MWAMBUSI - LEKULE

Breaking

17 Oct 2015

KUWA MSAIDIZI YANGA NI HATUA KWA MWAMBUSI

Kocha msaidizi wa Yanga Juma Mwambusi (kushto) akimuonesha kitu kocha mkuu wa timu hiyo Hans van der Pluijm
Kocha msaidizi wa Yanga Juma Mwambusi (kushto) akiwa sambamba na kocha mkuu wa timu hiyo Hans van der Pluijm


Msimu wa mwaka 2003-04 kocha Mholanzi Martin Jol alikataa ofa ya kuwa msaidizi wa Sir Alex Ferguson Manchester United na badala take kuendelea kuwa kocha mkuu wa klabu ya RCK Waalwijk ya Uholanzi.
Baada ya kuondokewa na msaidizi wake mreno Carlos Quiroz aliyehamia Real Madrid wakati huo, Martin Jol alikataa ofa ya kumsaidia Ferguson Manchester United.
Hali kama hiyo imetokea nyumbani Tanzania, ambapo baada ya kocha Charles Boniface Mkwasa kutakiwa na timu ya taifa, klabu ya Yanga ikamhitaji Mwambusi kuwa msaidizi wao kuziba nafasi iliyoachwa wazi na Mkwasa.
Tofauti na mholanzi Martin Jol, kocha Juma Mwambusi hakupepesa macho kujiunga na Yanga kuwa msaidizi hali akiacha nafasi ya ukocha mkuu wa Mbeya City.

Mjadala umekuwa ni mkubwa kwa wadau wa michezo nchini wakijaribu kuhoji usahihi wa Mwambusi kuhusiana na kuacha u-boss wa Mbeya City na kuwa msaidizi wa kocha mkuu wa Yanga.
Kuna kitu lazima tuwekane sawa hapa; mfumo wa soka letu ni tofauti kabisa na soka la barani Ulaya. Katika ligi yetu, na hali ilivyo halisi, hakuna uwiano kati ya vilabu kongwe nchini vya Simba na Yanga na vilabu vingine, Azam pekee.
Tofauti ya kimfumo kati ya ligi yetu na ligi zilizoendelea duniani ndiyo kitu kinachonifanya niamini kuwa Mwambusi yuko sahihi kwa maana ya kwamba kalamba dume ama galasa.
Hakuna tofauti kubwa ya kimaslai, wala fursa baina ya timu barani Ulaya na ndio maana klabu ndogo kamba Wimbledon ina mashabiki wake na wanapata fursa sawa na klabu nyingine yeyote.
Kwa Tanzania, tuende mbele turudi nyuma bado ufalme wa klabu za Simba na Yanga katika soka letu ni mkubwa sana. Ni ngumu sio tu kwa makocha, bali hata wachezaji kuzikatalia timu hizo zinapowataka.
Ili uonekane na upate changamoto na exposure ya kutosha kwa nchi yetu, lazima upitie Simba na Yanga, achilia mbali Azam ambao hivi sasa wamekamilika na kuzifikia klabu hizo ingawa bado linapokuja suala la ushabiki, bado Simba na Yanga ni wafalme wa soka ya bongo.
Kiuhalisia, kutoka Mbeya City kwa Mwambusi na kujiunga na Yanga ni hatua muhimu katika historia ya career take ya soka. Mwambusi sasa atafahamika, ataongeza ujuzi na kupata uzoefu wa kutosha kutokana na changamoto zilizopo katika klabu hizi kubwa tofauti na Mbeya City.
Bila shaka fursa aliyoipata kocha Boniface Mkwasa kuwa meneja wa timu ya taifa, imetokana na kiasi kikubwa uwezo na uzoefu alioupata akiwa kocha msaidizi wa Yanga.
Kesho hatujui nini kiko mbele ya Mwambusi kama ambavyo hatukujua kilichokua mbele ya Mkwasa.
Ingawa sitaki kuzungumzia masuala ya maslai ‘mtonyo’ ambao Mwambusi atanufaika zaidi akiwa Yanga tofauti na ilivyokua City, lakini hicho pia sio kitu cha kubeza hasa kwa maisha yetu ya kiswahili.
Profile ya Mwambusi sasa imeongeza kitu na kwamba inampa mwanya wa kuwa na fursa nyingi kubwa mbele yake kama ilivyomtokea Boniface Mkwasa ambaye sasa ni boss wa timu ya soka ya taifa ya kandanda ya Tanzania.
Mwisho nitumie fursa hii kumtakia kila la kheri mrithi was Mwambusi Mbeya City. Kuondoka kwa Mwambusi ni fursa kwake na kwamba ni wakati wa yeye pia kutengeneza jina lake katika ramani ya soka.

No comments: