ASAS : MKIMCHAGUA MWAKALEBELA IRINGA ITASONGA MBELE - LEKULE

Breaking

24 Oct 2015

ASAS : MKIMCHAGUA MWAKALEBELA IRINGA ITASONGA MBELE

Kada wa CCM ARIF Abri kushoto akipiga pushapu 
Kamanda wa Uvccm Mkoa wa Iringa Bw Salim Asas akizungumza na wananchi wa jimbo la Iringa Mjini 
ARIF akimwombea kura MWAKALEBELA 


Kamanda wa UVCCM Mkoa wa Iringa Salim Asas na Mjumbe wa Mkutano mkuu wa Taifa CCM Bw Arif Abri wamesema wapo tayari kuleta maendeleo ya jimbo la Iringa kwa kushirikiana na Frederick Mwakalebela kuwa mbunge wa jimbo la Iringa mjini
Wakimwombea kura leo Mwakalebela katika uwanja wa Mwembetogwa wakati wa ufungaji wa Kampeni za CCM , walisema wapo tayari Kama wafanyabiashara wakubwa Mjini Iringa kushirikiana na MWAKALEBELA kuleta maendeleo yaliyosimama kwa miaka mitano.
Asas alisema inasikitisha kwa kuona wananchi wa jimbo hilo wakitabika kwa kukosa mitaji wakati jimbo hilo lilikuwa na mbunge na kuna mfuko wa jimbo ambao ungeweza kusaidia mikopo nafuu.
Hata hivyo alisema kwa upande wake amekuwa akisumbuliwa na vijana kwa kuomba kusaidiwa baada ya kukosa msaada toka kwa mbunge wao .
Hivyo alisema iwapo watampa nafasi ya kuwa mbunge Bw Mwakalebela Wananchi wategemee maendeleo makubwa zaidi na kwa upande wake atashirikiana na Mbunge Mwakalebela kuleta maendeleo .
Huku kwa upande wake Abri alisema akiwa ni mmoja kati ya wadau wakubwa wa maendeleo jimboni hapo atahakikisha anafanya Kazi ya kuleta maendeleo na Mwakalebela.

Abri alisema kuwa suala la maendeleo jimboni hapo linahitaji mbunge makini Kama Mwakalebela na si vinginevyo .

No comments: