TANZANIA YASHIKA NAFASI YA TATU KATIKA UWAZI WA BAJETI KWA NCHI ZA A.MASHARIKI - LEKULE

Breaking

10 Sept 2015

TANZANIA YASHIKA NAFASI YA TATU KATIKA UWAZI WA BAJETI KWA NCHI ZA A.MASHARIKI


Meneja wa Program wa Haki Elimu,Godfrey Bonaventura akizungumza na waandishi wa habari juu ya utafiti uliofanywa na International Budget Partinership leo jijini Dar es Salaam,Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Haki Elimu,John Kalage
Mkurugenzi Mtendaji wa Haki Elimu, John Kalage akizungumza na waandishi wa habari leo wakati wa utoaji wa Uwazi wa Bajeti katika utafiti uliofanywa na Interntional Budget Partinaship iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam.kushoto ni Meneja Program wa Haki Elimu, Godfrey Boneventura (picha na Chalila Kibuda Globu ya Jamii)
Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii
TANZANIA imekuwa ya tatu katika nchi za Afrika Mashariki katika uwazi bajeti kwa wananchi kwa kupata alama 46.
Utafiti huu umefanywa kwenye nchi 142 ambazo zimesaini kuingia katika uwazi wa bajeti kwa wananchi ambazo hufanyika kila baada ya miaka miwili.
Akizungumza na waandishi wa habari Meneja wa Programu wa Haki Elimu,Godfrey Bonavetura amesema kutokana na Tanzania kupata alama 46 inatakiwa kutoa taarifa za bajeti kwa wakati.
Nchi ya Uganda nidio inayoongoza katika uwazi wa bajeti kwa kuwa na alama ikifuatiwa na Kenya kwa kuwa na alama 48 hali ambayo inafanya Tanzania kuongeza kasi katika uwazi wa utoaji bajeti.
Amesema Tanzania ni nchi ya tatu kutokana na kutoa taarifa chache za bajeti na kutoa mara kwa mara inaondoa ufisadi kwani wananchi wana kuwa uaminifu wa serikali wa serikali yao kutokana na taarifa zinazopatikana katika bajeti.

No comments: