Taarifa ya Magereza kukanusha uvumi wa tangazo la ajira - LEKULE

Breaking

30 Sept 2015

Taarifa ya Magereza kukanusha uvumi wa tangazo la ajira


Katika siku za hivi karibuni, kumekuwepo na tangazo kuhusu nafasi za ajira katika Jeshi la Magereza linalodaiwa kuwa limetolewa na Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza na kusambazwa kwenye baadhi ya Mitandao ya kijamii. Umma unajulishwa kuwa taarifa hizo siyo za kweli.

Jeshi la Magereza linapenda kuufahamisha umma kuwa ajira hutolewa na kutangazwa kupitia Vyombo vya Habari pamoja na tovuti ya Jeshi la Magereza ya www.magereza.go.tz na si vinginevyo

Hivyo, Jeshi la Magereza linawatahadharisha Wananchi wote kuwa macho na mitandao ya kitapeli inayotoa taarifa za kupotosha na kuleta usumbufu mkubwa kwani mfumo wa ajira ndani ya Jeshi la Magereza ni wa wazi na unafuata Kanuni na Taratibu za ajira za Utumishi wa Umma.

Imetolewa na kusainiwa na,
John C. Minja
KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA

29 Septemba, 2015