Mgombea Ukawa atumia muda mwingi kutambulisha familia - LEKULE

Breaking

8 Sept 2015

Mgombea Ukawa atumia muda mwingi kutambulisha familia


MGOMBEA (1)-001
Mgombea udiwani wa Kata ya Kilakala kwa tiketi ya Chadema , Mapunda Lusewe akitambulisha familia yake jukwaani.
Na Dustan Shekidele, Morogoro
MGOMBEA udiwani wa Kata ya Kilakala kwa tiketi ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kwa baraka za muungano wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), Mapunda Lusewe, Jumamosi iliyopita alizindua kampeni kwa kuibua minongo’no kufuatia kitendo chake cha kutumia muda mrefu kutambulisha familia yake jukwaani.
MGOMBEA (2)-001…Akimtambulisha mwanaye.
Lusewe alipanda jukwani sambamba na familia yake ya watu watano na yeye mwenyewe wa sita ambapo ni watoto wake wanne, akiwemo mmoja wa miezi tisa na mke.
MGOMBEA (3)-001…Akimtambulisha mkewe.
Hata hivyo, baadhi ya wananchi waliouhudhuria mkutano huo walionekana kupinga kitendo cha mgombea huyo kwa kushirikiana na mkewe, Herieth Fungo kumtoa mtoto huyo mchanga na kumnadi jukwaani majira ya saa 12 kasoro jioni ambapo baridi kali ilivuma kutoka Milima ya Uluguru iliyopo jirani kabisa na eneo hilo la mkutano.
MGOMBEA (4)-001“Hii jamani si haki. Kwanza ametumia muda mrefu kutambulisha watoto wake… yaani muda wa kunadi sera yeye anashughulika na familia yake jukwaani,” alisema mtu mmoja bila kutaja jina lake.
MGOMBEA (5)-001Akaendelea: “Halafu si mbaya mgombea kupandisha familia jukwaani, hata Rais Obama (wa Marekani) aliwahi kufanya hivyo. Lakini si kutumia muda mrefu.
“Kingine ni yule mtoto. Unajua ni saa kumi na mbili kasoro sasa. Baridi ya Milima ya Uluguru yote inamwingia, wangeangalia na hilo.”
Pamoja na yote, mgombea huyo alisema akichaguliwa kuwa diwani wa kata hiyo ataleta maendeleo huku wananchi wakimshangilia.

No comments: