MFUMO WA UTUNZAJI WA TAARIFA ZA VITUO VYA AFYA TANZANIA BARA WAZINDULIWA LEO JIJI DAR - LEKULE

Breaking

10 Sept 2015

MFUMO WA UTUNZAJI WA TAARIFA ZA VITUO VYA AFYA TANZANIA BARA WAZINDULIWA LEO JIJI DAR

 Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Donani Mmbando  akizungumza na waandishi wa habari hawapo pichani juu ya  Mfumo unahifadhi na kutoa taarifa za zituo vya Afya kituo tangu kinapojengwa, atakikifunguliwa na hata kinapofungwa, leo Jjijini Dar es salaam.
 Wanahabari wa kimsikiliza kwa makini Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Usitawi wa Jamii Donani Mmbando leo jijini Dar es salaam.
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Donani Mmbando akifafanua jambo leo Jjijini Dar es salaam.
 Mkuu wa Kitengo cha Tehama wa Wizara ya Afya na Usitawi wa Jamii Hermes Rulagirwa towa ufafanuzi kwa waandi wa habari juu ya mfumo wa kuhifadhi taarifa za vituo vya huduma za afya vya serikali na binafsi leo jijini Dar es salaam.
 SehemU ya wananchi walio hudhulia kikao hicho leo jijini Dar es salaam.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Donani Mmbando  akiwa katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbail leo Jjijini Dar es salaam .

WIZARA ya Afya na Ustawi wa Jamii imetengeneza mfumo wa kuhifadhi taarifa za vituo vya huduma za afya vya serikali na binafsi “Health Facility Registry (HFR) System”.
 
Mfumo unahifadhi na kutoa taarifa za kituo tangu kinapojengwa, ili kimejengwa, kufunguliwa na hata kinapofungwa. Zaidi tunapata taarifa ifutayo;-
Idadi ya vituo Tanzania bara, taarifa za kijiografia (yaani“Geographic coordinates), mahali kituo kilipo, kwa ngazi ya Mkoa, Wilaya, Mtaa/kijiji, umiliki, hali ya utendaji kazi yaani “operation status” na huduma inayotolewa na kituo. 
Kutokana na kukamilika kwa mfumo huu, naagiza Taasisi zetu kama NHIF, MSD, NACP, TFDA pamoja na wadau wengine waanze kutumia mfumo huu.
Mfumo huu umetengnezwa kwa ufadhiri wa mfuko wa ukimwi kifua kikuu  (Global fund) CDC, RTI Intenational. Pia natambua Ushiriki wa wadau wetu, University Computing Centre, Chuo kikuu cha Dar es salaam.
Aidha mfumo huu umetengenezwa kwa kushirikisha idala zote za Wizara na Taasisi zake. Hivyo ni mfumo shirikiskishi na una ownership.
Nawapongeza pia wajumbe wa kamati ya Afya za Mikoa na Wilaya, kwa kufanikisha, ukamilikaji wa mfumo huu.
Naagiza kwenu nyinyi waganga Wakuu wa Mikoa na Wilaya, kuhakikisha mnasimamia kwa kuingiza taarifa kwa wakati.

Baada ya kusema hayo, natangaza kuwa mfumo huu wa mfumo wa utunzaji wa taarifa za vituo vya afya tanzania bara, umezinduliwa rasmi.

No comments: