Tusikubali Kuvurugwa Tuwe Makini Tufanye Maamuzi Sahihi - LEKULE

Breaking

12 Jun 2015

Tusikubali Kuvurugwa Tuwe Makini Tufanye Maamuzi Sahihi


  Watanzania wameonywa kuwa makini kwa kutokubali kuvurugwa na watu wanaotangaza nia ya kugombea Urais katika uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu, badala yake wafanye maamuzi sahihi kwa kumchagua kiongozi atakayekuwa tayari kulinda rasilimali za nchi na asiye mpenda rushwa. 
 
Kauli hiyo imetolewa na Benard Membe   wakati akitafuta wadhamini  mkoani Ruvuma ambapo wanachama zaidi ya elfu tano walijitokeza kumdhamini. 
 
Aidha aliwaomba  wananchi wachague mtu ambaye  atakuwa na uzalendo wa  nchi na  ambaye atalinda  rasilimali za nchi  na kusimamiapia asiwe penda rushwa. 
 
Mgombea huyo amesema ,iwapo wataridhika kuwa yeye ndiye mwenye uwezo wa   kuongeza  watanzania zaidi ya milioni 45  hawana budi kumchangua. 
 
Katika hatua nyingine mgombea nafasi ya uraisi makongoro Nyerere pia aliwataka watanzania  kuwa makini na wagombea na wawasikilize na badaye wachague mtu ambaye ataweza kulinda chama na masirahi  ya watanzania

No comments: