Msajili avinyoshea kidole vyama vya siasa, ataka viheshimu Sheria ya Uchaguzi - LEKULE

Breaking

17 Jun 2015

Msajili avinyoshea kidole vyama vya siasa, ataka viheshimu Sheria ya Uchaguzi

Msajili wa vyama ya Siasa nchini, Jaji Francis Mtungi akizungumza wa waandishi Dar s Salaam jana kuhusu gharama ya sheria za uchaguzi mkuu wa mwezi Oktoba. Kushoto ni Msajili Msaidizi gharama za uchaguzi na Elimu kwa umma, Piencia Kiure.


Dar es Salaam.
Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi amevitahadharisha vyama vya siasa kuzingatia Sheria ya Gharama za Uchaguzi wakati mchakato wa kutafuta wagombea ukiendelea.
Mutungi alionya kuwa mwanasiasa yeyote atakayekiuka sheria hiyo atawekewa pingamizi wakati wa uteuzi ndani au nje ya chama.

Alisema ofisi yake itachukua hatua dhidi ya ukiukwaji wa sheria hiyo kama itajiridhisha na ushahidi utakaotolewa. Hata hivyo, alisema hawezi kuzungumzia mchakato wa kutangaza nia unaoendelea sasa kwa sababu bado wanafuatilia mwenendo wa wanasiasa.
“Ofisi yangu ni mwangalizi na msimamizi wa sheria hii, kwa hiyo tuna jukumu la kuhakikisha sheria inafuatwa,”alisema.

Kifungu cha 24 (2) cha Sheria ya Gharama za Uchaguzi, kinasema mgombea yeyote, au wakala wake, au chama chake kikihusika kuvunja masharti yaliyotajwa katika sheria hiyo basi mgombea huyo au chama kitaondolewa katika hatua ya uteuzi au uchaguzi.

Msajili Msaidizi, Kitengo cha Gharama za Uchaguzi na Elimu kwa Umma, Piencia Kiure alisema Kifungu cha 14 cha Sheria hiyo kinasema gharama zote za wagombea zitabebwa na chama husika. “Sheria inataka chama kutumia chini ya Sh2 bilioni ngazi ya rais na majimbo gharama italingana na ukubwa na idadi ya watu katika jimbo husika,” alisema Kiure.

No comments: