Amama Mbabazi atampinga rais Museveni - LEKULE

Breaking

15 Jun 2015

Amama Mbabazi atampinga rais Museveni

Raisi Museveni
 Waziri mkuu wa zamani wa Uganda Amama Mbabazi atampinga rais Yoweri Museveni kuwania tikiti ya urais wa chama cha NRM.
Bwana Amama Mbabazi anataka kuwania kiti cha urais dhidi ya mwandani wake wa zamani katika uchaguzi utakaokuwa mwakani.
Kupitia kwa taarifa aliyoichapisha kwenye mtandao wa Youtube, bwana Mbabazi aliahidi
''kufufua na kuleta muamko mpya nchini Uganda.''
Rais Museveni ametawala Uganda tangu mwaka wa 1986 na anatarajiwa kuwania urais kwa muhula wake wa nne.

Amama Mbabazi

Museveni alimfuta kazi bwana Mbabazi mwaka uliopita katika hatua iliyotafsiriwa na wachanganuzi wa kisiasa nchini humo kuwa mbinu ya kukandamiza mpinzani wake mkuu.
Bwana Mbabazi anakabiliwa na changamoto kubwa ya kushinda uteuzi katika chama tawala cha National Resistance Movement (NRM).
Rais Museveni tayari ameidhinishwa na kamati kuu ya chama japo anahitaji kupokea ithibati ya wanachama katika mkutano mkuu wa wajumbe.
Iwapo atakonga nyoyo za wajumbe wa NRM sasa Mbabazi sasa atawania urais dhifi ya Museveni
Mwandishi wa BBC Rachael Akidi anasema kuwa hii ndiyo itakayokuwa mtihani mkubwa zaidi kuwahi kumkabili rais Museveni ndani ya chama cha NRM.

No comments: