Msafara wa baiskeli Dar Es Salaam - LEKULE

Breaking

15 Jun 2015

Msafara wa baiskeli Dar Es Salaam


Mamia ya waendesha baiskeli walijitokeza kwenye msafara katika barabara za mji wa Dar es Salaam kwa lengo la kuhamasisha wananchi kutumia zaidi usafiri huo kwa ajili ya afya bora huku wakiitaka serikali kupinga uonevu unaofanywa na waendesha magari ambao husababisha ajali za barabarani.
Huu ni mwaka wa tisa sasa msafara huu umekuwa ukifanyika jijini Dar es salaam
Mbali ya kuwa ni tukio la burudani baina ya marafiki na familia, msafara huu una ujumbe maalumu
"msafara huu ni wito kwa serikali na wadau wa miundombinu kutenga sehemu mahususi ya kupitisha baiskeli"

Dar es Salaam ina watumia barabara zaidi ya laki tatu .
Mwenyekiti wa muungano wa vyama vya waendesha baiskeli mjini Dar es salaam UWABA Mejah Mbuya ,anasema idadi ya watumia baiskeli wanaofariki kutokana na ajali za barabarani ni asilimia 6 vifo vyote vitokanavyo na ajali barabarani.
''Anasema kuwa siku hii ni kubwa kutokana na kutokuwepo kwa waoneaji wa magari, lakini anatamani hali hii ingekuwa ni ya kila siku''
Hata hivyo, waandaaji wamesema tayari mabadiliko yanaonekana ndani ya miaka mitano iliyopita.

 Anasema kuwa ''serikali imekuwa pamoja nao katika mipango yao ya miundombinu mijini kwa sababu ya misafara hii, na kuwa punguzo la vifo vya waendesha baiskeli''.
Shughuli hii inalenga kuondoa dhana kwamba ni chombo cha usafiri kwa watu maskini.
Na ukiangalia watu wanaotumia baiskeli siku hizi , unaona mambo yameanza kubadilika.
Utaona watu wenye uwezo wa kati na wale wa juu nao wameanza kuutumia.

No comments: