Mgonja Kuanza Kujitetea Leo.......Anatuhumiwa kwa Matumizi Mabaya ya Ofisi na Kuisababishia Serikali Hasara ya Bilioni 11.7 - LEKULE

Breaking

19 May 2015

Mgonja Kuanza Kujitetea Leo.......Anatuhumiwa kwa Matumizi Mabaya ya Ofisi na Kuisababishia Serikali Hasara ya Bilioni 11.7

ALIYEKUWA Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Uchumi, Gray Mgonja anatarajia kuanza kujitetea leo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa kwa tuhuma za matumizi mabaya ya madaraka na kuisababishia Serikali hasara ya Sh  bilioni 11.7.
 
Washtakiwa hao walipanda kizimbani jana mbele ya Mahakimu Wakazi Sam Rumanyika na Saul Kinemela, wakati kesi hiyo ilipokuja kwa ajili ya Mgonja kuanza kujitetea.

Mgonja hakuweza kujitetea na kesi iliahirishwa hadi leo kutokana na Mwenyekiti wa Jopo la Mahakimu watatu wanaosikiliza kesi hiyo, Jaji John Utamwa, kushindwa kufika mahakamani hapo.

Kwa mara ya mwisho, kesi hiyo ilipangwa kwa utetezi kuanzia jana hadi Mei 29, mwaka huu.

Mgonja na aliyekuwa Waziri wa Fedha, Basil Mramba na Waziri wa Nishati na Madini, Daniel Yona, wanakabiliwa na kesi hiyo, iliyoko katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

Mramba, Yona na Mgonja wanakabiliwa na mashtaka 11 ya matumizi mabaya ya madaraka na kuisababishia serikali hasara ya Sh bilioni 11.7 kutokana na kutoa msamaha wa kodi kwa Kampuni ya Alex Stewart.
 

Mshtakiwa wa kwanza Mramba na wa pili Yona walikwisha kumaliza kutoa ushahidi katika kesi hiyo.

No comments: