Ukweli kuhusu ajali ya gari iliyoua Watu 2 na kujeruhi 16 Dar, usiku wa jana… - LEKULE

Breaking

14 Mar 2016

Ukweli kuhusu ajali ya gari iliyoua Watu 2 na kujeruhi 16 Dar, usiku wa jana…


Moja ya stori zilizochukua headline usiku wa March 13 2016 ni pamoja na hii ya ajali ya basi la Leina Tours lililoanguka maeneo ya Kimara Bucha, Dar es salaam na taarifa zake zikitolewa tofauti na baadhi ya watu.ajaliii
Leo March 14 2016 Kamanda wa Polisi Kanda maalum ya Dar es salaam Simon Sirro amelitolea ufafanuzi sahihi na kusema>>
Jana tarehe 13/3/2016 majira ya saa 3 na robo usiku, gari lenye namba T 878 CAH Scania Bus lilikuwa linatoka Kahama na kuja Dar es salaam, wakati likiwa kwenye barabara ya Dart mbele yake kulikuwa na gari aina ya Rav4 likija uso kwa uso
Wakati analikwepa bahati mbaya gari likamshinda na dereva kwahiyo akaenda kugongana na costa ya abiria, katika ajali hiyo tumewapoteza watu wawili akiwemo dereva wa basi lililokuwa likitoka Kahama pamoja na abiria mmoja
Lakini madereva wa magari mawili, Rav 4 na costa hadi sasa hawajapatikana, taarifa tulizonazo ni kwamba wale majeruhi wengine hadi sasa bado wanaendelea vizuri na tunawaombea waweze kupona

No comments: