Suarez aisawazishia Uruguay dhidi ya Brazil - LEKULE

Breaking

26 Mar 2016

Suarez aisawazishia Uruguay dhidi ya Brazil



Luis Suarez alifunga bao la pili na kuisawazishia Uruguay katika kipindi cha pili katika droo ya 2-2 dhidi ya Brazil katika mechi yake ya kwanza ya kimataifa tangu apigwe marufuku kwa kumng'ata mchezaji mwenzake katika kombe la dunia la mwaka 2014.

Mshambuliaji huyo wa Barcelona alikuwa hajaichezea Uruguay katika mechi ya kimataifa kwa takriban siku 640 kabla ya mechi ya kufuzu ya kombe la dunia siku ya Ijumaa.
Douglas Costa aliifungia Brazil baada ya sekunde 39 kabla ya Renato Augusto kuongeza uongozi huo katika dakika ya 26.

No comments: