Picha 15: Barabara ya Mwananyamala Dar, imefikia hapa baada ya RC Makonda kutoa siku 14 za adhabu - LEKULE

Breaking

26 Mar 2016

Picha 15: Barabara ya Mwananyamala Dar, imefikia hapa baada ya RC Makonda kutoa siku 14 za adhabu



Siku ya March 11 2016 Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda alifanya ziara ya kutembelea katika maeneo mbalimbali ya Wilaya ya Kinondoni kujionea  kero za uharibifu wa miundombinu ikiwepo barabara na kuamua kutoa agizo kwa Manispaa ya hiyo kuhakikisha inafanya ukarabati wa maeneo yaliyoharibika ndani ya siku 14 kabla ya kuwawajibisha.
Leo March 25 ripota wa millardayo.com aliongozana na mkuu huyo wa mkoa katika mitaa tofauti ikiwa ni pamoja na barabara ya Mwananyamala ili kujionea hatua zilizofikiwa na kukuta ukarabati ukiendelea…
Lakini bado mkuu wa mkoa hakuonyesha kuridhishwa na kazi iliyokuwa ikiendelea na kusema>> ‘Nilitoa siku 14 ukarabati wa hii barabara uwe umekamilika, nashukuru leo nimepita na nimekuta kazi imeanza, lakini nimewataka wahusika waangalie uwezekano wa kuwa na barabara za kudumu kwa muda mrefu‘ ;-Paul Makonda
Kuna barabara pale Makumbusho wamejenga alafu wameharibu mitaro, sasa nimemtaka mkandalasi arudi haraka na arekebishe, maana wamejaza mchanga kwenye mitaro, hatuwezi kuwa na barabara zisizokuwa na mitaro, baada ya siku kumi nitarudi tena kuhakikisha kama wamekamilisha‘ ;-Paul Makonda
AW1A9356
Barabara ya kutokea Makumbusho kuelekea Mwananyamala
AW1A9359
Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda wakati akikagua barabara
AW1A9361
Hiki ni kipande cha barabara ambacho bado hakijafanyiwa marekebisho
AW1A9364
Wafanyakazi wakiendelea kupiga kazi
AW1A9367
AW1A9368
Hapa huruhusiwi kupita wakati ujenzi ukiendelea
AW1A9371
Jamaa kataka kupenya wakamrudisha alipotoka
AW1A9375
Watu wakipiga kazi
AW1A9377
Jamaa akizibua moja ya mtaro ulioziba kwa uchafu
AW1A9379
Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda akicheki maendeleo
AW1A9388
AW1A9390
Barabara ya Mwananyamala sokoni
AW1A9395
Barabara imefungwa ili kuzuia watu wasipite kuharibu utaratibu wa kazi
AW1A9397
Mifereji pia imesafishwa kuondoa uchafu
AW1A9404
Baada ya kuhakikisha kazi inaenda, mkuu wa mkoa na watu wake wakipiga stori

No comments: