Mkuu wa Mkoa wa Arusha Adai Yeye Ndo Mwanzilishi wa Wazo la Kuhakiki Silaha Kabla ya Paul Makonda wa Dar - LEKULE

Breaking

26 Mar 2016

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Adai Yeye Ndo Mwanzilishi wa Wazo la Kuhakiki Silaha Kabla ya Paul Makonda wa Dar


MKUU wa Mkoa wa Arusha, Felix Ntibenda amesema kazi ya kuhakiki silaha iliyoanza kwa wakazi wa Dar es Salaam, ilishaanza mkoani mwake takribani miezi miwili iliyopita na kwamba ndiyo maana matukio ya kihalifu kwa Arusha yamepungua.

Ntibenda alisema hayo jana katika kikao cha Baraza la Ushauri la Mkoa wa Arusha na kusema yeye ndiye mwanzilishi wa wazo la kilichoazishwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda hivi karibuni.

Alisema wakati wakisubiri kuapishwa katika viwanja vya Ikulu, Dar es Salaam aliwaeleza wakuu wa mikoa jinsi alivyofanikiwa kudhibiti uhalifu kwa kuwataka wakazi wa Jiji na mkoa wa Arusha kuhakiki silaha zao.

‘’Kazi inayofanywa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ni wazo langu kwani sisi Arusha si mnaona uhalifu umepungua kwa asilimia kubwa sana? Hiyo ni kwa sababu wengi wana silaha, lakini si mali zao,’’ alisema.

Akizungumzia ulinzi, Ntibenda alisema hiyo inatokana na jitihada za kamati ya ulinzi na usalama kuthibiti kwa kiasi kikubwa uhalifu na matukio yasiyokuwa na amani na sasa Jiji la Arusha liko katika hali ya utulivu wa hali ya juu.
Alisema katika kipindi cha Januari mwaka jana hadi Desemba mwaka jana, jumla ya magunia 270 ya bangi yenye uzito wa kilo 2,500 na ekari 25 za mashamba ya bangi yaliteketezwa kwa kuchomwa moto.

Mkuu huyo alisema operesheni hiyo ilifanyika katika vijiji vya Imbibya, Ngarelaoni, Kisimiri Juu na Oldonyosambu na watuhumiwa 180 walikamatwa na kesi 160 zilifikishwa mahakamani.


Akizungumzia zuio la kutocheza `Pool’ saa za kazi, Ntibenda alisema wakuu wa wilaya na wakurugenzi ni lazima washiriki kikamilifu kupiga vita mchezo huo kuchezwa wakati wa kazi kwani ni jukumu la kila mmoja hapa na sio la mtu mmoja mmoja.

No comments: