13 Mar 2016
New
ALIKIBA NA SAUTI SOL WAUMALIZA UTATA WA KOLABO
Baada ya kundi linaloundwa na vijana
wanne wenye uwezo mkubwa wa kuimba kutoka nchini Kenya maarufu kama
Sauti Sol kuachia wimbo wa Uncondinationally Bae walioshirikiana na
msanii nyota kutoka Tanzania maarufu kama Alikiba, umepokelewa vyema na
mashabiki wao huku kukiwa na maswali juu ya ngoma hiyo.
Sauti Sol ndio walikuwa wakwanza kupost
kupitia mitandao ya kijamii hususani Instagram na Youtube juu ya wimbo
huo ambapo awali ulikuwa ukisomeka Sauti Sol FT Alikiba jambo ambalo
lilizua utata kwa mashabiki kwa kuwa na sintofahamu juu ya nyimbo hiyo
huku wakijiuliza hiyo ni nyimbo ya pamoja au Alikiba ndiye
aliyeshirikishwa.
Jambo
lililozidi kuwatia hofu mashabiki wa msanii Alikiba ni kutoona post
yeyote ya msanii huyo kuhusu ngoma hiyo mpya, jambo ambalo siyo kawaida
yake pale anapokuwa ametoa ngoma mpya
Kwa kuzingatia hayo mtembezi.com ilipiga
story na moja ya watu wa karibu na Alikiba na akaueleza mtandao huu
kuwa hiyo ngoma ni ya pamoja siyo kwamba Alikiba kashirikishwa hivyo
watakapo badilisha ndio wataanza kuiunga mkono kazi hiyo.
Mtembezi iliendelea kusubiria
kitakachojiri huku ikiendelea na pitapita yake mtandaoni na kukutana na
Post ya Alikiba iliyorekebishwa na kuandikwa Sauti Sol and Alikiba
tofauti na awali ilikuwa inaonesha kuwa yeye ndiye aliye shirikishwa,
halikadhalika kwa upande wa Sauti Sol nao wamebadilisha.
Haya sasa Kenya, zamu yetu!! Tanzania let’s go!!!!#UnconditionallyBae with my brothers@sautisol x officialalikiba#SautiSolAlikiba #LetsUnite Link in bio ameandika Alikiba kupitia ukurasa wake wa Instagram.
About SOSTENES LEKULE JR
Hi, I`m Sostenes, Electrical Technician and PLC`S Programmer.
Everyday I`m exploring the world of Electrical to find better solution for Automation. I believe everyday can become a Electrician with the right learning materials.
NEWS
Subscribe to:
Post Comments (Atom)








No comments:
Post a Comment