Toka Bungeni: Nyumba 3500 Kujengwa kwa Ajili ya askari Polisi - LEKULE

Breaking

1 Feb 2016

Toka Bungeni: Nyumba 3500 Kujengwa kwa Ajili ya askari Polisi

Serikali inakamilisha taratibu zakupata mkopo toka serikali ya China bilioni 500 kwaajili ya ujenzi wa nyumba 3500 za askari wa jeshi la polisi nchini kufikia mwaka 2025.

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi Masauni Yusufu Masauni ameyasema hayo leo mjini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Tunduma Mheshimiwa Frank Mwakajoka aliyetaka ufafanuzi wa lini serikali itaboresha na kuongeza nyumba za askari polisi nchini.

Naibu Waziri Masauni amesema kuwa ni dhamira ya serikali kuhakikisha jeshi la polisi linaboresha makazi na kuwa na ofisi ili kuwezesha utoaji wa huduma kwa wananchi kuwa mzuri na pindi mkopo huo utakapo kamilika ujenzi utaanza kwa Tanzania Bara na Zanzibar.


Naibu Waziri huyo ameongeza kuwa kwa sasa wapo katika mpango wa awali wa kujenga nyumba 350 nchi nzima ambazo zitatatua tatizo hilo la walinzi wa raia na mali za wa Tanzania kukosa makazi bora na ya kudumu.

No comments: