Kundi La Mziki La Navy Kenzo Latoa Wimbo Na Video Mpya-kamati - LEKULE

Breaking

1 Feb 2016

Kundi La Mziki La Navy Kenzo Latoa Wimbo Na Video Mpya-kamati

THE INDUSTRY MUSIC LABEL
Baada ya kutamba Mwaka Jana Africa nzima na wimbo unaoitwa ‘Game’, Kundi la Navy Kenzo limeanza mwaka vizuri baada ya kutoa wimbo mpya pamoja na video yake unaoitwa “Kamatia” .
 Wimbo huo umeshaanza kuwa gumzo sehemu mbali mbali na kuonyeshwa kwenye TV za kimataifa siku mbili tu baada ya kutoka.
 Uzinduzi wa Wimbo Huo ulifanyika Kiaina yake kwa Staili ya ‘Flash Mob’ Kwenye Club ya Rhapsody kwa kuwasuprise waliokuwa ndani ya Club hiyo.
 
Kundi la Navy Kenzo linaloundwa na Aika na Nahreel ,mpaka sasa wameshatoa nyimbo kadhaa zilizotamba sana kama Moyoni, Bokodo, Visa na nyingine nyingi.
 
Navy Kenzo wameamua kutoa Wimbo pamoja na Video yake moja kwa moja kutokana na ushindani uliopo kwa sasa kwenye Music wa Bongo Flava.
Video imefanyika nchini South Africa na Muongozaji wa Video wa kimataifa anayeitwa Justin Campos.
 
==>Bonyeza Link ifuatayo Kudownload Wimbo huo ;DOWNLOAD AUDIO

==>Au Angalia Video Hapa;VIDEO

No comments: