Ofisi ya Uhusiano, Kitengo cha Masoko TANESCO waelimisha umma - LEKULE

Breaking

25 Feb 2016

Ofisi ya Uhusiano, Kitengo cha Masoko TANESCO waelimisha umma

 Baadhi ya wanafunzi wa Chuo cha VETA NJIRO, waliohudhuria kwenye mafunzo ya usalama na wizi wa umeme wa kwanza (Kushoto) ni Afisa Huduma kwa wateja Bw. Juma Msuya.
 Mwanafunzi wa Chuo cha Veta kilichopo Oljoro mkoani Arusha akiuliza swali kwa wataalamu wa TANESCO katika mafunzo hayo.
 Baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Msingi  Oldonyo Sambu ya Mkoani Arusha wakiwa na zawadi zao walizopewa na wataalam wa TANESCO kama zawadi za kushiriki vyema katika mafunzo hayo na kujibu na kuuliza maswali, kushoto ni Afisa Mahusiano na Wateja Mkoa wa Arusha Bw.Fred Mbavai.
 Baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Msingi Mbweni ya jijini Dar es Salaam wakiwa tayari kuwapokea wataalam kutoka TANESCO kwa ajili ya kupokea elimu kuhusu masuala mbalimbali ya umeme.
  Afisa Masoko  Bi. Jenifer Mgendi kutoka Shirika la Umeme (TANESCO)     akitoa zawadi kwa wanafunzi waliojibu maswali vizuri wakati wa utoaji elimu ya masuala ya umeme, katika Shule ya Msingi Tandika ya jijini Dar es Salaam.

Baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Msingi Kisukuru ya jijini Dar es Salaam, wakishangilia zawadi walizopewa wakati wa wataalam kutoka TANESCO walipotoa elimu ya masuala ya umeme. Katikati ni Afisa Uhusiano Bi.salama Kasamalu.

No comments: