Mbowe Atangaza Baraza lake la Mawaziri Bungeni Leo - LEKULE

Breaking

5 Feb 2016

Mbowe Atangaza Baraza lake la Mawaziri Bungeni Leo

Kiongozi mkuu wa kambi ya upinzani bungeni Freeman Mbowe ametangaza baraza lake la mawaziri kivuli leo bungeni mjini Dodoma.


Mbowe, ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Hai na Mwenyekiti wa Chadema ametaja baraza lake ambalo litakuwa na lengo la kuishinikiza serikali ya Rais Magufuli kutimiza kile alichoahidi kwa Watanzania.

Baraza hilo ni kama ifuatavyo;


1.Wizara ya Ofisi ya Rais, Tamisemi, Utumishi na Utawala Bora.

Mawaziri – Jaffar Michael

Naibu Waziri – Joseph Nkundi na Ruth Mollel

2.Wizara ya Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Waziri – Ali Saleh Abdalla

Naibu Waziri – Pauline Gekul

3.Ofisi ya Waziri Mkuu: Sera, Bunge, Kazi Vijana, Ajira na Walemavu

Waziri – Esther Bulaya

Naibu – Yusuph Makame na Maftah Abdalla

4.Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

Waziri – Magdalena Sakaaya

Naibu Waziri – Emmaculate Swari

5.Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.

Waziri-Inj. James Mbatia

Naibu Waziri Willy Kombucha

6.Wizara ya Fedha na Mipango

Waziri – Halima Mdee

Naibu Waziri – David Silinde

7.Wizara ya Nishati na Madini

Waziri – John Mnyika

Naibu Waziri – John Heche

8.Wizara ya Katiba na Sheria

Waziri – Tundu Lissu

Naibu Waziri Abdalla Mtolela

9.Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afika Mashariki, Kikanda na Kimataifa.

Waziri – Peter Msigwa

Naibu Waziri – Riziki Shaghal

10.Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

Waziri – Juma Omari

Naibu Waziri Mwita Waitara

11.Wizara ya Mambo ya Ndani

Waziri – Godbless Lema

Naibu Waziri Masoud Abdalla

12.Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi.

Waziri – Wilfred Lwakatare

Naibu Waziri – Salum Mgoso

13.Wizara ya Maliasili na Utalii

Waziri Esther Matiko

Naibu Waziri– Cecilia Pareso

14.Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji.

Waziri Anthony Komu

Naibu Waziri Cecil Mwambe

15.Wizara ya Elimu, Sayansi Teknolojia na Ufundi

Waziri – Suzan Lyimo

Naibu Waziri Dkt. Ali Suleiman Yusuph

16.Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

Waziri – Dkt. Godwin Mollel

Naibu Waziri Zubeda Sakul

17.Wizara ya Habari, Utamadu, Wasanii na Michezo

Waziri – Joseph Mbilinyi

Naibu Waziri – Devotha Minja

18.Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Waziri – Hamidu Hassan

Naibu Waziri– Peter Lijualikali



No comments: