DK.KIGWANGALLA AHIMIZA JAMII KUWA NA UTAMADUNI WA KUPIMA AFYA ZAO MARA MWA MARA - LEKULE

Breaking

29 Feb 2016

DK.KIGWANGALLA AHIMIZA JAMII KUWA NA UTAMADUNI WA KUPIMA AFYA ZAO MARA MWA MARA

dk hk
Naibu Waziri wa Afya, Dk. Kigwangalla akitoa hutuba fupi wakati wa tukio hilo la kambi maalum ya matibabu ya bure kwa wananchi wote iliyoandaliwa na Care Foundation kwa kushirikiana na wadau wengine akiwemo Mbunge wa jimbo la Ilala, Mh. Mussa Hazan Zungu.
Naibu Waziri wa Afya, Maendejana ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kigwangalla amehimiza Jamii kuwa na utaratibu wa kupima afya mara kwa mara katika hali ya kubaini matatizo yanayowakabili ilikuchukua hatua ikiwemo kupata tiba mapema
Dk. Kigwangalla ametoa kauli hiyo mapema jana Februari 28.2016, jijini Dar es Salaam, wakati alipokuwa mgeni rasmi katika kambi maalum ya kupima afya bure kwa wananchi mbalimbali wakiwemo wa Jimbo la Ilala kwa kuandaliwa na Care Foundation na wadau wengine wa afya ikiwemo Hospitali ya Ebrahim Haji Chartable Health Centre ambao wanasimamia kutoa huduma za matibabu kwa kushirikiana na taasisi zingine.
Akitoa hutuba yake fupi, kwa wananchi mbalimbali walifika katika tukio hilo la kupatiwa matibabu hayo ya bure, Naibu Waziri, Dk. Kigwangalla amesema Jamii wanatakiwa kuwa na maisha yenye afya hivyo zoezi la kupima afya mara kwa mara ni bora zaidi kaika kuimalisha afya ya mwili.
“Wananchi wapo na wakati mwingi wakifanya shughuli zingine na hata muda kupima afya inakuwa ngumu. Kukinga ni bora Zaidi kuliko tiba. Zoezi hili litasaidia sana wananchi wengi na tunaomba muendelee na maeneo yote ya nchi yetu.” Ameeleza Dk.Kigwangalla.
Aidha, Dk. Kigwangalla amempongeza Mbunge wa Jimbo la Ilala, Mussa Hazan Zungu kwa kuwezesha kuandaa zoezi hilo kwa kushirikiana na wadau hao kwani ni mfano bora wa kuigwa na wabunge wengine pindi wapatapo nafasi ya kutumikia jamii iliyowachagua.
Pia katika zoezi hilo, Mbune wa jimbo la Ilala, Mh. Mussa Zungu na Naibu Waziri Dk. Kigwangalla walipata wasaha wa kupima afya zao pamoja na kutembelea maeneo ya kutolea huduma na kushuhudia namna huduma zinavyotolewa kwa wananchi.
Kambi hiyo ya matibabu, inatoa matibabu hayo bure kwa wananchi wote wanaofika hapo ambapo pia mbali na matibabu wanatoa huduma ya dawa huku wakitoa pia mawani kwa watu wenye matatizo ya macho. Watu mbalimbali wamekaribishwa kupatiwa matibabu hayo ambayo pia yanatolewa na madaktari bingwa wa magonjwa husika.

yi
Tukio likiendelea
DK KIGWANGALLA 65
Naibu Waziri wa Afya, Dk. Kigwangalla akiwa katika meza ya kupima afya ya mwili ikiwemo magonjwa yasio ambukiza kama vile Magonjwa ya moyo, sukari, shinikizo la damu na mengine mengi katika zoezi linaliendelea katika viwanja vya Bustani ya jiji iliyopo mkabara na Ukumbi wa Karimjee.
Dk. Kigwangalla
Naibu Waziri wa Afya. Dk.Kigwangalla akiwa katika vipumo hivyo..
DK
Mbunge wa Ilala, Mh. Mussa Hazani Zungu, akipima afya katika zoezi hilo..
TIBA 3
Dk. Efrahim Mika Zaky wa Msimbazi Eyes Vision Center, (kushoto) akimpima macho mmoja wa wananchi waliojitokeza katika zoezi hilo linaloendelea jana jijini Dar es Salaam katika viwanja vya Bustani ya jiji, mkabara na Ukumbi wa Karimjee.
TIBA
Uchunguzi wa macho ukiendelea..
TIBA3
Dk. Efrahim Mika Zaky wa masuala ya macho, akimpima macho Naibu Waziri wa Afya, Dk. Kigwangalla wakati wa zoezi hilo..
TIBQ667
Naibu Waziri wa Afya Dk. Kigwangalla akiwa katika kupima macho kwenye kambi maalum ya kutoa huduma za matibabu ya bure yaliyoandaliwa na Care Foundation na wadau wengine katika viwanja vya Bustani ya Jiji, Posta Jijini Dar es Salaam.
TIBA222
Naibu Waziri Dk.Kigwangalla akiwa katika moja ya sehemu ya kutolea dawa na miwani kwa watu watakaobainika kuwa na matatizo katika macho..
DK KIGWANGALLA 685
Naibu Waziri akipokea ua maalum kama ishara ya kukaribishwa katika ufunguzi huo wa kambi maalum ya matibabu ya bure yaliyoandaliwa na CARE Foundation na wadau wengine akiwemo Mbunge wa jimbo la Ilala, Mussa Hazzan Zungu.

No comments: