Ajali ya ndege ya Urusi Misri: Sissi akubali kuwa lilikua shambulizi - LEKULE

Breaking

25 Feb 2016

Ajali ya ndege ya Urusi Misri: Sissi akubali kuwa lilikua shambulizi


Picha zilizopigwa na Wizara ya Dharura ya Urusia mbapo kunaonekana ndege ilioanguka katika mji wa Wadi al-Zolomat, Misri tarehe 1 Novemba.
Picha zilizopigwa na Wizara ya Dharura ya Urusia mbapo kunaonekana ndege ilioanguka katika mji wa Wadi al-Zolomat, Misri tarehe 1 Novemba.
Na RFI
Rais wa Misri Abdel Fattah al-Sisi amekubali kwa mara ya kwanza Jumatano hii kwamba ndege ya watalii ya Urusi ambayo iliangushwa Oktoba 31 katika eneo la Sinai na kuua watu wote 224 waliokuemo, kilikua kitendo cha shambulio, kama ilivyoelezwa mapema na Urusi.
Tawi la kundi la Islamic State nchini (IS) lilikiri kuhusika na shambulio hiyo siku hiyo hiyo, na kuthibitisha baadaye kwamba ilikuabomu dogo lililowekwa ndani ya ndege hiyo, lakini mpaka wakati sasa Cairo ilikua ikisema na kurejelea kwamba sababu za ajali hazijulikani.
"Yeyote yule alieidungua ndege hiyo, alikua anatafuta nini? Kuwashambulia tu watalii (nchini Msri)? Hapana, kuweka hatarini uhusiano wetu na Urusi," Rais Sissi amesema mbele ya umati wa viongozi wa serikali na biashara wakati wa mkutano kuhusu maendeleo ya Misri, mkutano ambao umerushwa hewani kwenye runinga mbalimba nchini Misri.
Siku kumi baada ya ajali, Moscow, kupitia sauti ya Rais Vladimir Putin mwenyewe, alitangaza kuwa wapelelezi wake kwenye eneo la tukio walibaini kwamba ndege hiyo iliangushwa kwa shambulio, na kupiga marufuku ndege zote za Urusi kusafiri kwenda Misri hadi itakapotangazwa tena. Uingereza ilipiga marufuku ndege zake zote kusafiri kwenda kituo cha mapumziko cha Sharm el-Sheikh, ambapo ndege ya Urusi iliruka ikipaa hewani. Wakati huo huo Uingereza kama Urusi, iliwarejesha nyumbani raia wake wote waliokuwepo katika mji huo wa mapumziko.
Sekta ya Utalii, ambayo tayari imekabiliwa na wimbi la mashambulizi nchini Misri iko hatarini. London, mpaka sasa haijaruhusu ndege zake kusafiri kwenda katika mji wa Sharm el-Sheikh, wala Moscow kuruhusu ndege zake kusafiri kwenda nchini Misri.

No comments: