TRA Yasitisha Upokeaji Wa Maombi Ya Nafasi Za Kazi - LEKULE

Breaking

30 Jan 2016

TRA Yasitisha Upokeaji Wa Maombi Ya Nafasi Za Kazi

ISO 9001:2008 CERTIFIED
KUSITISHWA KWA MUDA UWASILISHWAJI WA MAOMBI YA KAZI
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ilitoa tangazo la nafasi za kazi katika magazeti mbalimbali ambapo waombaji wanatakiwa kuwasilisha maombi kupitia tovuti ya TRA.
 
Kutokana na maombi ya nafasi za kazi kuingiliana na shughuli za kulipa kodi mwisho wa mwezi kupitia tovuti, TRA inasitisha kwa muda upokeaji wa maombi ya kazi kupitia tovuti hadi Jumanne tarehe mbili Februari 2016 ili kuruhusu ulipaji wa kodi uendelee bila usumbufu.
 
Pia TRA imeongeza muda wa kupokea maombi hadi tarehe 17 Februari 2016.
 
Waombaji wote wa nafasi za kazi zilizotangazwa wanaombwa kutuma maombi yao kuanzia Jumanne tarehe mbili Februari 2016.
 
Tunaomba radhi kwa usumbufu wowote utakaojitokeza kutokana na mabadiliko haya.
 
Kwa maelezo zaidi tafadhali wasiliana na:
kituo cha huduma kwa wateja- 
08000780078, 0800750075, 0713800333

Limetolewa na:
Idara ya Huduma na Elimu kwa Mlipakodi

TRA-Makao Makuu

No comments: