Taarifa Ya Kukanusha Uvumi Wa Kuwepo Ajira Za Madaktari JWTZ - LEKULE

Breaking

30 Jan 2016

Taarifa Ya Kukanusha Uvumi Wa Kuwepo Ajira Za Madaktari JWTZ


Hivi karibuni kumekuwa na uvumi unaoeleza kuwa JWTZ limetoa nafasi za kazi kwa vijana wenye fani ya Udaktari na kuwataka vijana hao kuripoti Makao Makuu na vyeti vyao kwaajili ya usaili.

Habari hizo si za kweli,JWTZ kama zilivyo taasisi nyingine za serilikali lina mfumo rasmi wa kutangaza habari zake hivyo jeshi linawaomba wananchi wazipuuze taarifa hizo.

Aidha JWTZ linawataka wamiliki wa mitandao ya kijamii kutotoa taarifa za jeshi bila kuwasiliana na Makao Makuu ya jeshi kinyume na utaratibu huu,unawasababishia wananchi usumbufu usio wa lazima.

Imetolewa na Kurugenzi ya Habari na
Uhusiano Makao Makuu JWTZ.

No comments: