Rais Magufuli AMFUKUZA Kazi Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Kwa Utovu wa Nidhamu - LEKULE

Breaking

16 Jan 2016

Rais Magufuli AMFUKUZA Kazi Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Kwa Utovu wa Nidhamu


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ametengua uteuzi na kumfukuza kazi Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Bw. Faisal Issa kutokana na utovu mkubwa wa nidhamu aliouonesha katika kikao cha kamati ya ulinzi kilichofanyika  tarehe 15 Januari, 2016 Mjini Mwanza.

Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue amesema Rais Magufuli amechukua hatua hiyo baada ya kupokea taarifa ya yaliyotokea katika kikao cha kamati ya ulinzi cha Mkoa, kilichoongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Magesa Mulongo.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU.
Dar es salaam

15 Januari, 2016

No comments: