Polisi wapatiwa mafunzo maalum ya usalama barabarani - LEKULE

Breaking

18 Jan 2016

Polisi wapatiwa mafunzo maalum ya usalama barabarani

Polisi 1
Mtaalamu wa Matairi kutoka Kampuni ya TBL Group, Peter Muthee,  akiwalezea Maofisa  wakaguzi wa Jeshi la Polisi  Kikosi Usalama Barabarani jinsi ya kutambua matairi yaliyo na athari za kiusalama wakati wa mafunzo maalumu kwa maofisa hao yaliyofanyika  jijini Dar es Salam mwishoni mwa wiki.
-Yametolewa na kampuni ya TBL Group
Polisi 2
Maofisa wa polisi kutoka kitengo cha  usalama barabarani wakibadilishana mawazo na mtaalamu wa matairi kutoka TBL wakati mafunzo maalumu kwa maofisa hao yaliyofanyika jijini Dar es Salam mwishoni mwa wiki.(P.T)

polisi 4
Mkufunzi wa madereva  kutoka Kampuni ya Bia TBL, Hubert Kubo  akizungumza na Maofisa  Wakaguzi wa Jeshi la Polisi Kikosi Usalama Barabarani wakati wa mafunzo maalumu kwa maofisa hao yaliyofanyika  jijini Dar es Salam mwishoni mwa wiki.
tbl police 1
Afisa wa polisi Kikosi Usalama Barabarani Smax Ibrahim akitoa mada juu ya usalama wakati wa mafunzo hayo  yaliyofanyika  jijini Dar es Salam mwishoni mwa wiki.
TBL 7
Mkurugenzi wa Mafunzo wa TBL Group,Gaspar Tesha akitoa mada wakati wa mafunzo hayo.
TBL police 6
Katika mafunzo hayo yatakayofanyika mikoa mbalimbali polisi pia walishiriki zoezi la kufundisha zoezi la ukaguzi wa magari kama wanavyoonekana wakiangalia mmoja wa wafanyakazi wa kampuni hiyo akikagua gari.

No comments: