Polisi wa
Ufaransa wanachunguza gari lililochomwa moto mbele ya hoteli ya
Splendid katika mji wa Ouagadougou, Burkina Faso, Januari 17, 2016.
Na RFI
Baada ya
mashambulizi dhidi ya hotli ya Splendid na mgahawa wa Cappuccino
katikati mwa mji mkuu wa Burkina faso, Ouagadougou siku ya Ijumaa usiku,
wachunguzi wanaendelea na kazi ngumu ya kuwatambua watu 29 waliouawa
katika shambulio hilo.
Mpaka sasa giza bado linatanda kuhusu namna operesheni ya vikosi vya usalama ilivyoendeshwa.
Mwendesha
mashitaka wa Mahakama Kuu ya Ouagadougou, Maïza Sérémé, ametoa sehemu
ya orodha ya watu waliopoteza maisha katika mashambulizi hayo ya kigaidi
yaliyolenga hoteli ya Splendid na migahawa ya Cappuccino na Taxi
Brousse.
Kati ya
wahanga 29 waliohesabiwa, saba bado hawajatambuliwa, ikiwa ni pamoja na
watu wanne weusi na wazungu watatu. Kati ya wahanga 22 waliotambuliwa,
kuna wanne kutoka Canada, saba wa Burkina Faso, wawili kutoka Ukraine,
Mfaransa mmoja mwenye asili ya Ukraine, Wafaransa wawili, wawili kutoka
Uswisi, mmoja kutoka Libya, mmoja kutoka Marekani, mmoja kutoka Uholanzi
na mmoja kutoka Ureno.
Mwendesha
mashitaka, katika taarifa yake ya pili, amefahamisha raia na familia za
wahanga kwamba uchunguzi wa kitabibu unaendelea na taarifa ijayo
itawaitisha kuendelea na zoezi la kuwatambua wahanga na kuondolewa kwa
miili yao.
Kukusanya ushahidi
Kuhusu
uchunguzi, timu ya kiufundi bado ipo katika eneo la mashambulizi.
Hairuhusiwi mtu yeyote kuingia katika sehemu kulikotokea mashambulizi.
Maafisa wa polisi wanaendelea kukusanya vitu vyote ambavyo vinaweza
kusaidia katika uchunguzi huu.
No comments:
Post a Comment