Kardinali Pengo Aruhusiwa Kutoka Muhimbili - LEKULE

Breaking

22 Jan 2016

Kardinali Pengo Aruhusiwa Kutoka Muhimbili


Askofu Mkuu wa Jimbo Katoliki la Dar es Salaam Mwadhama Kardinali Polycarp Pengo aliyekuwa amelazwa katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete, Muhimbili ameruhusiwa baada ya afya yake kuimarika.

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa taasisi hiyo, Profesa Mohammed Janabi alisema jana kuwa Kardinali Pengo aliruhusiwa saa 6.30.

Awali, Profesa Janabi alisema Kardinali Pengo alilazwa katika kitengo hicho mwaka jana kabla ya kuruhusiwa siku 10 baadaye baada ya kupata nafuu na alipewa siku tisa kurudi hospitalini hapo kwa ajili ya kuendelea kufuatilia zaidi afya yake.


Kardinali Pengo alilazwa katika kitengo hicho Desemba 31 mwaka jana na kuruhusiwa siku 10 baadaye. Januari 18 alirudi hospitalini hapo kwa ajili ya matibabu ya ufuatilizi kabla ya jana kuruhusiwa. 

No comments: