Jocktan Maluli ‘MAKEKE’: Msanii wa mitindo anayevuma nje ya mipaka ya Tanzania - LEKULE

Breaking

25 Jan 2016

Jocktan Maluli ‘MAKEKE’: Msanii wa mitindo anayevuma nje ya mipaka ya Tanzania

12345680_1816488911911612_3268924740048111556_n
Msanii wa mitindo Jocktan Cosmas Maluli maarufu kama Makeke (katikati) akiwa katika moja ya majukwaa ya fashion la  Slum fashion Africa lililofanyika nchini Kenya.
Na Andrew Chale, Modewjiblog
 Makeke ni msanii wa mitindo ambaye anafanya  mitindo ya kiafrika/kiasili kutokana na maisha ya Muafrika halisi, Jina kamili ni Jocktan Cosmas Maluli amabaye pia ni mmiliki wa kampuni ya MAKEKE AFRIKA CO.LTD  iliyopo Boko  – Dar es salaam ambayo ilianzishwa mapema mwaka  Desemba 2012.
Mpaka  sasa jina la MAKEKE  limeweza kutumika kama jina na brand ya kibiashara inayomtambulisha Jocktan Maluli ambaye hadi sasa ofisi yake  hiyo ikiweza kufikisha umri wa zaidi ya miaka 5 huku ikiwa na idara tatu muhimu amabazo ni MAKEKE AFRIKA KOLEKSHENI, MAKEKE MEDIA & MAKEKEMODELING AGENCY.
 Makeke  anabainisha kuwa, alikuwa na kipaji cha uchoraji tangu akiwa mdogo, na alishawahi kuwa mchoraji bora wa shule ya msingi wakati huo akiwa Mbeya.  Kipaji hicho aliendelea nacho na hata kidato cha nne na kidato cha sita alipoibuka kuwa mchoraji bora wa katuni Nyanda za juu kusini na Tanzania kwa ujumla.
383428_509985679048913_109316577_n
Moja ya mitindo inayobuniwa na msanii wa mitindo nchini, Makeke.
Katika uchoraji bora huo  aliwahi kuzawadiwa  kiasi cha pesa na cheti na taasisi ya kuzuia rrushwa TAKUKURU, wakati huo akiwa kidato cha tano na cha sita ndipo alipoanza kufanya mitindo kama ‘Model’ na akafanikiwa kuwa Mr. Mbalizi high school wakati huo na Mr. Mbeya vijijini hapo ndipo alipopewa jina la ‘Model Makeke’  kutokana na miondoko yake jukwaani, baadae alianza kushauriwa na watu kuwa kutokana na uwezo mkubwa wa kuchora anaweza kuwa mbunifu mzuri wa mavazi basi toka hapo ndo akaanza rasmi ubunifu wa na watu walikuwa wakikubali kazi zake.
Baadae akafanikiwa kujiunga na chuo kikuu cha Dododma (UDOM) ambapo alikuwa akisomea Shahada ya (FINE ARTS & DESIGN) na hapo ndipo haswa alipotimiza ndoto zake za kuwa msanii bora wa mitindo, baadae akajiunga na AFRIKA SANA chini ya mbunifu  Alilnda Sawe kwa ajili ya mazoezi ya vitendo.
Makeke katika kufikia malengo yake  ameweza kutimiza ndoto yake huku akiwa  Mbunifu wa nguo, ubunifu wa mapambo ya ndani pamoja na kupamba kuta, graphics design, make up design.
11014980_778535628860582_2970655073466105500_n
Mitindo inayobuniwa na Msanii wa mitindo nchini, Makeke.
Anabainisha kuwa, na uwezo wote huo: “Ni  kwa sababu toka nikiwa mdogo nilikuwa katika mazingira hayo ya kujifunza vitu vingi, na pia chuo kikuu tulikuwa tukisoma aina mbali mbali za sanaa”. Anabainisha Makeke.
Anaongeza kuwa: “Kikubwa nafkiri watu bado hawajaelewa vile mimi nafanya mambo yangu, na pia hawajaelewa hichi kitu nnachokiita sanaa ya nguo, kiukweli sipendi kuitwa ‘Designer’  napenda mtu aniite ‘artist’, kwa hiyo ‘Am a fashion artist’ nafanya kitu kwa uwezo zaidi ya ule wa ‘Designer’,  sababu ‘designers’  wengi wamekuwa watu wa ku copy na ku pest (bandika bandua) yaani hawaumizi kichwa
 katika kufanya michoro yao, mimi sina mipaka katika kufanya nguo naweza tengeneza nguo katika mazingira yoyote kwa material yeyote.  Pia watu bado hawajanielewa kwasababu nafanya mitindo migumu ingekuwa ni muziki basi ni muziki wa Tamaduni (Culture music) nguo nyingi si rahisi kuvalika mtaani.” Anaeleza Makeke.
Akifafanua juu ya  tasnia ya mavazi pamoja na soko lake: Makeke anabainisha kuwa,  Tasnia  ya mitindo Tanzania iko katika matabaka  ambapo anabainisha kuwa, Wapo wanamitindo wanaojiona kama miungu watu  na wabinafsi hali ambayo wanarudisha nyumba tasnia nzima ya mitindo hapa nchini.
11692649_1623035417913743_1040310650842835408_n
“Mimi sipendi mambo ya majigambo na ubinafsi. kitu ambacho sikipendi  na ndio maana niko mbali na watu wa tabia hiyo na hii ndo sababu ya kwenda kufanyia mitindo nje ya Tanzania mara kwa mara.  Huko nje watu wako makini na wanakuelewa  nini unafanya kuliko hapa  nyumbani” anaeleza.
Makeke kutokana na kufanya kazi zake nyingi  nje ya Tanzania  vyombo vingi vya habari vya ndani vimekuwa vikishindwa kumpa nafasi huku vingi vikiangalia watu waliokwisha toka na kujulikana zaidi. Kwa hali hiyo licha ya kuwa ni mchanga katika tasnia ya mitindo anaamini sasa ni zamu yake na Tanzania sasa inamuhitaji.
 Makeke mbali na kufanya ubunifu wa mavazi, . nje ya ubunifu anafanya:  Mambo ya upakaji rangi kuta, uchoraji wa katuni,  Upigaji wa picha za matukio na kuziwekea ubunifu zaidi,  kubuni vitu ikiwemo logo, matangazo ya mabango na vitu mbalimbali kwani anaamini hivyo vyote vinazama kwenye sanaa , na hii ndo maana ya kuitwa msanii kutokana na kuwa navyo tokea utoto wake na pia kuvisomea ngazi ya chuo kikuu.
12246646_1815745555319281_8068763822089450566_n
Makeke anaamini kuwa yeye yupo tofauti zaidi na wengine: “Tofauti kubwa ni kitu kimoja nakiita CREATIVE& ARTISTIC MINDS, nna uwezo wa kubuni na pia nna chembe chembe za kisanii ndani yangu ndio maana hata kazi  zetu hazifanani. Hata siku moja kazi yangu huwezi kukuta inafanana na mtu mwingine hasa wabunifu hawa wa hapa nyumbani” anaeleza.
Pia anaongeza kuwa, tofauti nyingine baina yake na wabunfu wengine ni   kwamba wao wanafanya mitindo kama kazi ya ziada lakini kwa yeye ni kazi ya kwanza na anaifanya kama mbobezi huku akiifanya kazi hiyo ya ubunifu kwa nyakati za sasa na baadae akimaanisha kuwa anamalengo ya mbali.
Hata hivyo, katika ubunifu wake wa mavazi, Makeke anaweka wazi kuwa,  amekuwa akibuni  kutokana na maisha ya muafrika  huku hasira na ndoto zake kubwa  ni kuona mavazi ya ubunifu yanabuniwa na kutoka   na yenye kuendana na msimu wowote ule. Makeke kwa sasa ana bidhaa sokoni   ‘BUTTERFLY BRAND’.
10993080_775821845798627_5962451429695722486_n
Kiwango cha elimu yake na mwaka:  Kidato cha nne (O level 2003 – 2006), Kidato cha tano na sita (Advance. 2007 -2009) elimu hiyo ya vidato vyote akiwa ameipatia katika shule ya Mbalizi High School iliyopo Mbeya Vijijini Mkoani Mbeya. Makeke  emezaliwa 18 Feb 1990).
Miongoni mwa kazi alizofanya kwenye majukwaa makubwa ya ubunifu na mitindo:
Majukwaa ya ndani ni pamoja na Mbeya Redds Nait, In forest fashion show-Mikumi, RRM fashion week, Marahaba fashion show, Lady in Red, Bagamoyo international festival of arts and culture (2014 na 2015). Pia Makeke ni  “Official dresser miss IFM 2013,  2014, and 2015”
Robi- Slum Fashion Africa, Kisumu  Fashion Week,  Fashion & Style  Expo- Nairobi. The Designer  walk ( Kenya) fashion show – TDWFS – (Afrika Kusini).
Kwa majukwaa ya nje ya Tanzania (International)  ni pamoja na : Slum fashion Africa, Picha fashion Festival, The designers walk fashion show, The reality tv fashion show, East African motor show.
Majukwaa mengine anayotarajia kupanda  hapo baaadae: Bongo style competition, East Africa Fashion week, Ekhulen fashion show based on SADC countries members, Abuja International Fashion.
Watu walio kwenye tasnia ya Ubunifu wanaomvutia ni pamoja na : Henrick Biscouvs (Scandnavia),Ken Kasea (Morogoro), Kipilyango  wa  Africa shiners Tz,  Ailinda Sawe (Tanzania)  na  Asia Idorous.
10450159_778535665527245_162580848044186168_n
Miongoni mwa ubunifu na mitindoanayotamba nayo, Makeke.
10285599_469480239851535_3678542762004401787_o
10298059_469480313184861_7961502346037653987_o
Baadhi ya mitindo ya ubunifu ya Makeke.
10991077_1575488776025325_6111997563711787786_n
mitindo hiyo anayobuni Makeke.
10991178_402725176563522_6362169284138556739_n

Msanii wa mitindo, Makeke akiwa katika moja ya mitindo yake..

No comments: