WAZIRI
wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto
amemsimamisha kazi Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi ya Saratani ya Ocean
Road, Dk.Diwani Msemo ili kupisha uchunguzi pamoja na mambo mengine ili
kubaini mgongano wa kimaslahi ulioathiri utendaji wa taasisi hiyo
chini ya kaimu mkurugenzi huyo.
Kwa
mujibu wa taarifa iliyotolewa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii,
Jinsia,Wazee na Watoto mwenye Wizara hiyo, Ummy Mwalimu imesema kuwa
kutokana na ziara alizofanya Rais Dk. John Pombe Magufuli inaonyesha
kukosekana kwa dawa katika hospitali za Serikali huku vituo vya afya
vya binafsi vikiwa na dawa.
Taarifa
ya Waziri huyo imesema kuwa upungufu wa dawa umeendelea kujitokeza kwa
karibu zaidi na baadhi ya wagonjwa walieleza kwa uchungu jinsi
wanavyopata dawa kwa tabu hatazile wanazotakiwa wapate kwa bei ya ruzuku
au zilezinazotakiwa kutolewa bure na serikali.
Kwa
msingi wa uwazi na uwajibikaji ameagiza watendaji wote wa sekta ya afya
hususani wakuu wa vituo vya kutolea huduma za afya, Wafamasia, Wauguzi
na Waganga Wafawidhi wa vituo vya kutolea huduma za afya kukiri kwa
maandishi kwa ngazi zao za uwajibikaji endapo wanamiliki Hospitali,
Zahanati, Kiliniki, Maduka ya Dawa ndani ya siku 21 kuanzia leo Desemba
23 mwaka huu ambapo agizo hilo limeotolewa.
Aidha taarifa hiyo imedai kuwa kufanya hivyo kutaziba mianya ya upotevu wa dawa na vifaa tiba katika vituo vya umma.
No comments:
Post a Comment