WAZIRI
MKUU Kassim Majaliwa amewaagiza Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya na
Wakurugenzi wa Halmashauri zote nchini kuhakikisha kuwa wanaongeza
udhibiti na usimamizi wa migogoro ya ardhi kwenye maeneo yao husika.
Ametoa
agizo hilo leo mchana (Jumatano, Desemba 23, 2015) wakati akizungumza
na viongozi wa mkoa wa Lindi kwenye Ikulu ndogo mara baada ya kuwasili
akitokea jimboni kwake Ruangwa.
“Ardhi
ni mali ya Serikali lakini maeneo yanayotwaliwa kwa sababu mbalimbali
za maendeleo yasiwe chanzo cha migogoro na wananchi tunaowaongoza,” alisema.
Akitoa
mfano, Waziri Mkuu alisema anatambua kuna mgogoro wa eneo la mgodi
katika wilaya ya Ruangwa baina ya wananchi na wawekezaji wa kampuni ya
Uranex. .....
"....Na
hii ni kwa sababu wao ndiyo waliamua kufanya tathmini (evaluation) ya
eneo hilo. Yale ni makosa kwa sababu aliyepaswa kufanya tathmini ni
Halmashauri na siyo mwekezaji,” alisema.
Alisema wawekezaji wanaruhusiwa kisheria kufanya tathmini lakini sheria waliyoitumia ni sheria namba 8 peke yake. “Kama
Halmashauri ingefanya kazi hiyo ni lazima wangetumia sheria ya ardhi ya
vijiji pamoja na sheria ya madini na wananchi wangepata thamani halisi
ya ardhi yao,” alisema.
“Ninaagiza
Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa ikahakiki lile eneo na kubaini kama ni
la kilimo au la madini na kama ni la kilimo, wananchi wamelima mazao
gani na kwa muda gani kisha wafanye tathmini upya. Yuko valuer wa
Halmashauri mwenye dhamana hiyo na siyo wao,” alisema.
“Nasisitiza
tena ni vema Wakurugenzi wote, Wakuu wa Wilaya chini ya uongozi wa
Wakuu wa Mikoa mjiridhishe kuwa hakuna migogoro kwenye maeneo yenu. Kama
ipo, imalizeni kwa kukaa mezani na kuzungumza na pande husika,
inawezekana kabisa,” alisisitiza.
No comments:
Post a Comment