Jaji Mark Bomani Amshauri Maalim Seif Akubali Uchaguzi Urudiwe - LEKULE

Breaking

18 Dec 2015

Jaji Mark Bomani Amshauri Maalim Seif Akubali Uchaguzi Urudiwe


JAJI Mkuu na Mwanasheria Mkuu Mstaafu, Mark Boman amesema kuwa Makamu wa Kwanza wa Rais wa Serikali ya Umoja Zanzibar, Maalim Seif Hamad akubali uchaguzi urudiwe Zanzibar kwani kama alishinda atashinda tena kutokana na waliompigia katika uchaguzi ulifutwa watampIgia kura tena.

Boman aliyasema hayo jana jijini Dar eS Salaam , wakati akizungumza na waandishi wa habari.Alisema kuwa Maalim kujitangazia kuwa ameshinda ni suala ambalo halikufuata utaratibu hivyo kutokana na mazingira hayo uchaguzi ufanyike ili kupata Rais wa Serikali ya Zanzibar.

“Kurudia uchaguzi Zanzibar ni jambo lisilo epukika lakini wakae na kuangalia dosari zilizojitokeza na kufuta uchaguzi ili  lishughukiwe kisheria, bila kufanya hivyo kunaweza kuleta matatizo” alisema Jaji Mstaafu, Boman.

Alisema kuwa uchaguzi uliofanyika Zanzibar walitakiwa kukaa na kuona wapi walikosea katika kuondoa changamoto hizo ambapo ilikuwa ngumu kutokana na Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar, Jecha Salum Jecha na wajumbe walishindwa kuafikiana.

Kuhusu suala la katiba mpya, Bomani alisema ni lazima lishughulikiwe kuanzia pale lilipoishia kwani kuachwa kwake ni aibu ya nchi kutokana na mabilioni ya fedha yaliyotumika katika mchakato huo.


Alisema migogoro ya wafugaji na wakulima inatokana na kutokuwa na katiba ambayo ndio ingekuwa suluhu ya utatuzi wa migogoro hiyo.

No comments: