BONANZA LA UZAZI WA MPANGO KWA VIJANA LAFANYIKA JIJINI DAR ES SALAAM - LEKULE

Breaking

13 Dec 2015

BONANZA LA UZAZI WA MPANGO KWA VIJANA LAFANYIKA JIJINI DAR ES SALAAM

 Mkurungezi Mkuu wa Marie Stopes Tanzania, Anil Tambay akizugumza na wananchi  (hawapo pichani)  kwenye bonanza la uzazi wa Mpango kwa vijana ambalo lilifanyika mwishoni mwa wiki katika viwanja vya Mwembeyanga,Temeke jijini Dar.
 Mgeni rasmi Zukrah Mkwizu akizungumuza na wananchi (hawapo pichani) kuhusiana na suala zima la Uzazi wa Mpango,na kusisitiza kuwa uzazi wa mpangp ni silaha imara ambayo vijana wanaweza kuitumia kupangilia maisha yao na kujikinga dhidi ya utoaji mimba usio salama na kulinda ndoto zao dhidi ya mimba zisizotarajiwa.
 Balozi wa vijana wa Marie Stopes , Doreen Benne akifafanua jambo mbele ya wakazi wa mji wa Temeke na viunga vyake waliofika kwenye kwenye Bonanza la Uzazi wa Mpango kwa Vijana lililofanyika mwishoni mwa wiki ndani ya viwanja vya Mwembeyanga, Temeke, Dar es Salaam.
 Mwanamuziki Barnabas Elias 'Barnaba akionesha umahili wake wa kulitawala jukwaa katika Bonanza la Uzazi wa Mpango kwa Vijana Mwembeyanga, Temeke, Dar es Salaam

Sehemu Ya Wananchi Waliofika Katika Bonanza La Uzazi Wa Mpango Kwa Vijana wakifuatilia yaliyokuwa yakijili kwenye bonanza hilo ndani viwanja vya Mwembeyanga, Temeke, Jijini Dar Es Salaam

No comments: