Baada ya kipigo, Van Gaal ajifukuza kabla ya kufukuzwa - LEKULE

Breaking

28 Dec 2015

Baada ya kipigo, Van Gaal ajifukuza kabla ya kufukuzwa

louis-van-gaal_1

Kocha wa Manchester United, Louis Van Gaal (pichani) ambaye kibarua chake kipo katika kipindi kigumu kufuatia kipigo cha goli 2 kwa bila kutoka kwa Stoke City amesema anafikiri anatakiwa kuacha kibarua cha kuinoa klabu hiyo.
Akiwa katika wakati mgumu wa hatma ya kibarua chake Van Gaal ameshudia timu yake ikifungwa goli 2 kwa bila na kuwa mchezo wa 7 kufungwa kwa msimu huu na kikiwa kipigo cha kwanza ndani ya miaka 54 Manchester United kufungwa siku ya Boxing Day huku ikiwa ipo nje ya timu nne za juu kwa Ligi Kuu ya Wingereza na kuwa imetolewa katika hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Ulaya UEFA.
Alipolizwa na kituo cha Sky Sports baada ya mchezo wa Manchester United na Stoke City kama uongozi wa Manchester United bado unampa ushirikiano Van Gaal alijibu “Ninaweza kuwa kimya mimi binafsi, hilo ni jambo ambalo nazungumza na Ed Woodward [mtendaji mkuu] kuhusu yeye na sio wewe [mwandishi],
“Sio lazima mpaka klabu inifukuze mimi, muda mwingine ninafanya maamuzi mwenyewe ya kuondoka, ninahitaji kwanza kuzungumza na bodi ya Manchester United na wafanyakazi wenzangu na hata wachezaji ila sio wewe”

Pia Van Gaal akalizwa kama ataendelea kuifundisha timu hiyo “Ni ngumu kwasababu nimekuwa sehemu ya kupoteza michezo minne, tumepoteza na watu wananiangalia mimi … natakiwa kushughulikia hilo lakini muhimu zaidi ni wachezaji kushughulikia sababu wao ndiyo wanaocheza na sasa ni jambo kubwa. Najaribu kufanya kila kitu lakini hali hii imeshakuwa kubwa na kubwa kila mchezo na tunatakiwa kushughulikia hilo”

No comments: