Uhamiaji Mkoa wa Singida yawakamata Warundi walioingia nchini kinyume cha sheria - LEKULE

Breaking

18 Oct 2015

Uhamiaji Mkoa wa Singida yawakamata Warundi walioingia nchini kinyume cha sheria

SAM_0110
Baadhi ya raia wa nchini Burundi walioingia nchini kinyume cha sheria wakiwa kwenye ofisi za idara ya Uhamiaji Mkoa wa Singida wakisubiri kurudishwa kwao wakiwa chini ya ulinzi wa askari wa kikosi cha uhamiaji

[SINGIDA] Idara ya Uhamiaji Mkoa wa Singida inawashikilia watu saba raia wa nchini Burundi waliokutwa wakiwa katika Mji mdogo wa Itigi,wilayani Manyoni kwa tuhuma za kuingia nchini kinyume cha sheria.
Afisa uhamiaji Msaidizi wa Mkoa wa Singida,Moses Mandago alisema watu hao raia wa nchini Burundi walikamatwa okt,saba,mwaka huu,baada ya idara hiyo kupata taarifa kutoka kwa raia wema za kuwepo kwa raia hao kwenye eneo la mji mdogo wa Itigi.
Aidha Mandago alifafanua kwamba madhumuni ya raia hao kutoka nchini Burundi lilikuwa kwenda Morogoro kufanya biashara,na kumtaja Amani Michael Horombile (18) kuwa ndiye aliyekwenda mpaka Burundi kuwafuata baada ya kutumwa na kaka yake aliyetambulika kwa jina la Medsoni Emanueli.
“Lakini hata hivyo walidai kwamba kuna mtu ambaye  anaitwa Amani Michael Horombile (18),kati ya watu hao saba ndiye aliyeenda mpaka Burundi akiwa ametumwa na kaka yake anaitwa Medsoni Emanueli ambaye anadai alikuwa anakaa Turiani,Morogoro”alisisitiza afisa huyo.
Kwa mujibu wa kaimu afisa uhamiaji huyo waliokamatwa kwa tuhuma za kuvunja sheria ya nchi ni pamoja na Alex Nintunze (15),Ibrahimu Leopold (25),Kubwimana Erike(21),Ibrahimu Jafar(17),Hakizimana Yoshuwa( (13),Kelvin Maliyamungu (14) na Amani Michael Horombile (18).
Watu hao kwa mujibu wa Mandago walitumia usafiri wa gari moshi kutoka Kigoma na walikuwa na tiketi zinazoonyesha wanakwenda Tabora lakini walipofika Itigi,ndipo TT wa gari la moshi aliwashitukia na baada ya kuwahoji walidai wanakwenda Dodoma na ndipo TT alipowashusha na kuwakabidhi kituo kidogo cha polisi Itigi.
Hata hivyo kaimu afisa uhamiaji huyo aliweka bayana kuwa walipofanya mawasiliano,ikabidi wamtoe afisa mmoja wa idara hiyo hadi Morogoro kwa lengo la kuutafuta mtandao unaojihusisha na kazi hiyo ya kuwasafirisha raia hao ili waweze kuusambaratisha.
“Kwa kushirikiana na maafisa uhamiaji wa Mkoa wa Morogoro wakasema yupo Dar-es-Salaam na hivyo ndipo afisa huyo aliondoka Morogoro kwenda Dar-es-Salaam,nia ikiwa ni kumkamata mtuhumiwa huyo ili aweze kutuonyesha watu hao ili tuweze kujua mtandao huo upo wapi”alisema.
 Kutokana na raia hao kutokuwa na vibali vya kuwaruhusu kuingia nchini,hivyo idara ya uhamiaji Mkoa wa Singida imechukua hatua za kuwafukuza nchini kwa kuwasindikiza hadi Mkoani Kigoma .
 Hata hivyo aliweka bayana kuwa matukio kama hayo katika kipindi cha mwaka 2014 hayakuwa ya kutisha sana kutokana na baadhi ya watu kutoka nchini Ethipia wanaoletwa na kutelekezwa na wenyeji wao kwenye magari.
Akizungumza kwa niaba ya wahamiaji hao,mmoja wa raia hao wa Burundi,Kelvin Maliyamungu alikiri kuwa wametokea nchini Burundi na walikuwa wakisafirishwa kwenda Mkoani Morogoro kufanyakazi ambayo hata hivyo hakuweza kuifahamu mpaka wakati huo.
SAM_0109
Wahamiaji hao wa  Burundi..
SAM_0118

jengo la Uhamiaji mkoa wa Singida..

No comments: