Dar es Salaam.
Wanafunzi 775,729 walioandikishwa kufanya mtihani wa darasa la saba nchini, kesho wanaanza kufanya mtihani huo, huku idadi ya watahiniwa ikipungua ukilinganisha na walioandikishwa mwaka jana.
Wanafunzi 775,729 walioandikishwa kufanya mtihani wa darasa la saba nchini, kesho wanaanza kufanya mtihani huo, huku idadi ya watahiniwa ikipungua ukilinganisha na walioandikishwa mwaka jana.
Akizungumza na waandishi
wa habari jijini hapa, Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani (Necta),
Dk Charles Msonde amesema masomo yatakayotahiniwa kesho na kesho kutwa
ni Kiswahili, Kiingereza, Sayansi, Hisabati na Maarifa ya Jamii.
Dk
Msonde amesema watahiniwa 748,514 watafanya mtihani kwa lugha ya
Kiswahili na watahiniwa 27,215 watafanya mtihani huo kwa lugha ya
Kiingereza ambayo wamekuwa wakiitumia kujifunzia.
“Watahiniwa
wasioona walioandikishwa kufanya mitihani ni 76 na watahiniwa wenye
uoni hafifu ambao wanahitaji maandishi makubwa ni 698, kati yao wavulana
ni 330 na wasichana ni 368,” alisema Dk Msonde.
Amesema
maandalizi ya mtihani huo yamekamilika ikiwa ni pamoja na kusambazwa
kwa fomu maalumu za kujibia mtihani (OMR) na nyaraka nyingine zinazohusu
mtihani huo. Alisisitiza kuwa mtihani huo unalenga kupima uelewa wa
wanafunzi kwa yale waliyojifunza katika kipindi cha miaka saba.
Katibu
huyo wa Necta alizitaka Kamati za Mikoa na Wilaya kuhakikisha kuwa
taratibu zote za mitihani zinazingatiwa ipasavyo ikiwa ni pamoja na
kuhakikisha kuwa mazingira ya vituo vya mitihani yapo salama, tulivu na
kuzuia mianya yote inayoweza kusababisha udanganyifu.
“Mtihani
huu ni muhimu kwa Taifa kwa sababu hutumika katika uchaguzi wa
wanafunzi wanaojiunga na elimu ya sekondari. Ni matarajio yetu kwamba
wanafunzi wataufanya mtihani huo kwa kuzingatia taratibu zote za mtihani
ili matokeo yaonyeshe uwezo wao,” alisema.
No comments:
Post a Comment